Thursday 22 August 2013

MWANAMKE AOKOLEWA BAADA YA KUTAKA KUJIRUSHA KUTOKA GHOROFA YA 7 NCHINI CHINA


Mwanamke mmoja  nchini China amenusurika kufa baada ya kuokolewa na Askari wa Kikosi cha Zimamoto alipotaka kujirusha kutoka ghorofa ya saba ya jengo lililopo nchini humo.
Askari alimuwahi mama huyo kabla hajajirusha na kumvutia pembeni. Tukio hilo limetokea jijini Tongren, nchini China juzi Jumatatu.
Video hapo juu inamwonyesha askari aliyekuwa amejifunga kamba kiunoni kwa ajili ya usalama akimwokoa mama huyo na kumpeleka sehemu salama kabla ya kukimbizwa hospitali kwa matibabu.

FAMILIA YA MASOGANGE YAMWACHIA MUNGU

FAMILIA ya Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ inadaiwa kumwachia Mungu ishu ya binti huyo kukamatwa na madawa ya kulevya Julai 5, mwaka huu nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa ndugu mmoja wa familia hiyo aliyeomba jina lake lisitiriwe, wameamua kumwachia Mungu ishu hiyo kwani ndiye anayejua ukweli.
“Unajua baba wa Masogange (mzee Gerald Waya) ni mlokole, sasa amekabidhi ishu nzima mikononi mwa Mungu kwa hiyo hayuko tayari kusemasema maneno ambayo hayatakuwa na faida,” alisema ndugu huyo.
Habari zinazidi kudai kwamba, mzee huyo aliwahi kuchukizwa na kitendo cha binti yake huyo kujiingiza kwenye sanaa, hadi kuonekana akinengua kwenye muziki.
Hilo liliwahi kubainishwa na Masogange mwenyewe miaka ya nyuma alipohojiwa na gazeti ndugu na hili (Ijumaa) kupitia safu ya Ten Questions (Maswali Kumi) ambapo ilikuwa hivi:
TQ: Inasemekana umetokea kwenye familia ambayo imeiva kidini, walokole, wao wanachukuliaje suala la wewe kuingia kwenye mambo ya kuuza sura tena wakati mwingine kwenye mavazi ya kimitego?
Agnes: Mh! Baba yangu hataki kabisa kusikia mambo ya muziki na niliwahi kukosana naye lakini nalazimisha kwa kuwa ni moja ya ajira.
Jitihada za kumpata baba wa Masogange ziligonga mwamba baada ya namba iliyotolewa na ndugu huyo kutokuwa hewani.
Masogange na nduguye, Mellisa Edward walikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, Afrika Kusini wakiwa na ‘unga’ kilo 150 aina ya crystal methamphetamine wenye thamani ya shilingi bilioni 6.8.

Feza in relationship,see what she is said.

















“Feza is my life partner and our relationship should not be grouped with other failed Big Brother Africa relationships,” proclaimed a proud O’Neal born Zibanani Madumo as his lover stood nearby. 

Likewise, Feza is equally feeling her man. With the innocence of a teenager finding love for the first time, she told the media: “I love O’Neal from Botswana.”
A lot of uncertainty has been flying around about whether the two who found each other during their stay in the reality television series will last the mile. However, their shared sentiments about each other will surely put to rest all those concerns.

To cement the fact that the two lovebirds mean business and are committed to their relationship, Botswana’s makoti, Feza, jetted into the country yesterday from Tanzania. Feza, who is a musician back home, will be in the country for an indefinite period. O’Neal, Feza and friend Motamma Sesinyi - who brought them together - were hosted by Botswana National Youth Council at Lansmore Hotel on the same day that Feza arrived in Gaborone. Wearing matching Timberland boots, the lovebirds walked into the press conference room casually holding hands and looking right at home in each other’s company. If there was any uncertainty over whether they would last, those rumours disappeared the minute the pair came in. During the course of the press conference, O’Neal’s shoulders would turn into a hiding place for the shy and petite Feza who would often hide behind her man.

Having seen them over the course of the show and how they both avoided to offend the public by being intimate on camera, one wonders what they did as a couple the first time they met outside the Big Brother house minus the cameras glued on them. 
Although they were both reluctant to divulge what they often did, according to the little information that they provided, they covered themselves with a Maasai blanket and kissed, they hastily said before changing the topic.

Prior to heading into the house, the two who each has a son were single. O’Neal has a seven-year-old boy whose mother, by his own admission, is still in good terms with. Feza’s son named Jaden is turning five in December. And when they entered the Big Brother house, finding a partner during the challenging period of their stay was the least of their concerns. The two were among the last people to get into a relationship. “We have fought a lot during the show and the fact that we are here together today is proof that we will overcome any challenge. Only God can say that this will work or not,” explained Feza, adding that she could not predict their future but that everything will happen in good time. The relationship has not only been blessed by Motamma but Feza’s mother back home has also given it the go ahead. “I spoke to my mother over the phone and the first thing she wanted to find out was whether I was serious or this was just a game,” she revealed.

Meanwhile, a fundraising dinner will be hosted tomorrow at the Gaborone International Convention Centre. The dinner hopes to raise funds for a cause that O’Neal holds dear to his heart - promoting a reading and learning culture among the youth.

Watanzania zaidi ya 100 wako gerezani nchini China kuhusiana na dawa za kulevya, 20 ni wanawake!

Kama kuna jambo ambalo linaichafua Tanzania katika jukwaa la kimataifa kwa siku hizi, basi ni tatizo la usafirishaji wa dawa za kulevya.
Zamani tatizo hili halikuwa kubwa sana, ni mtanzania mmoja mmoja sana alikuwa akikamatwa nje kwa kusafirisha dawa za kulevya. Kwa hiyo jina la nchi yetu lilikuwa linasikika mara moja moja sana au kwa bahati mbaya kuhusiana na tatizo la dawa za kulevya. Lakini katika siku za hivi karibuni tumesikia kuwa kuna watanzania wanakamatwa Ulaya, Amerika Kaskazini, Amerika Kusini, Asia na hata katika nchi za Afrika, kama ilivyotokea majuzi huko Afrika Kusini. Kwa sasa ukisikia jina la Tanzania linatajwa kuhusiana na tatizo la dawa za kulevya, si bahati mbaya tena na si mara moja moja kama zamani.
Serikali yetu imekuwa ikijitahidi sana kujenga jina zuri la Tanzania na kuitanganza Tanzania kuwa ni kisiwa cha amani, nchi yenye vivutio vingi vya utalii na yenye ukarimu kwa wageni. Na kweli kama ukitembelea nchi yoyote yenye watu wanaoifahamu Tanzania, si vigumu kusikia Tanzania ikisifiwa, lakini kama ukiona mtu amekaa kimya, basi ujue kuna uwezekano kuwa hataki kutaja suala la dawa za kulevya.
Mwanzoni nilikuwa naamini kuwa watanzania ni watu wenye maadili ambao wanapokwenda nje ya nchi wanakumbuka kuwa “mabalozi wazuri” wa nchi. Lakini baada ya kutembelea sehemu mbalimbali duniani, hasa nchi za Asia na Asia Kusini Mashariki, na kukutana na wenyeji na kuwauliuza mtazamo wao kuhusu Tanzania na watanzania, nikagundua kuwa sifa zote nzuri za Tanzania zinafunikwa na sifa mbaya moja au mbili. Kubwa ni tatizo la dawa za kulevya, na nyingine ni ukahaba (Hong Kong).
Pamoja na kuwa ni watanzania wachache sana wanaosafirisha dawa za kulevya, ni hao wachache ndio wanaofanya jina la watanzania wengine walio wengi lichafuke, na kuwafanya watanzania wanaokwenda nje ya Tanzania kwa malengo halali, kama vile biashara, michezo na hata utalii, wakumbwe na matatizo wasiyostahili.
Zamani nilikuwa ninakasirika sana ninapotolewa kwenye mstari wa uwanja wa ndege na kuanza kupekuliwa na kuulizwa maswali ‘ya kipuuzi’, kana kwamba mimi ni mhalifu au mtuhumiwa wa uhalifu. Nilikuwa najihisi kuwa mimi ni mhanga wa ubaguzi wa rangi, kitu ambacho sikutegemea kutoka kwa nchi marafiki zetu. Kuna wakati hata nilifikia hatua ya kukwaruzana na maofisa wa uwanja wa ndege, kwa kuona wananitendea isivyostahili. Lakini baadaye baada ya kuangalia hali halisi na kuona matendo yanayofanywa na baadhi ya watanzania wanaokuwa nje ya Tanzania, nikagundua kuwa wasiwasi walionao maofisa wa viwanja vya ndege vya nchi za Asia kuhusu watu wenye pasi za kusafiria za Tanzania, ni wa haki na unaeleweka, si ubaguzi wa rangi na si ubaguzi dhidi ya watanzania. Kama ni ubaguzi wa rangi, basi matendo ya baadhi yetu ndio yanawapa kisingizio cha kufanya hivyo.
Kinachonifanya nisione kuwa ni ubaguzi wa rangi ni kuwa, nchini China kwa mfano kuna adhabu kali sana kwa watu wanaokamatwa kwa makosa ya dawa za kulevya, wachina wengi wamehukumiwa adhabu ya kifo. Lakini cha ajabu ni kuwa watanzania wanaokamatwa kwa makosa sawasawa na wanayofanya wachina, wanapewa vifungo virefu na adhabu ya kifo, lakini hadi sasa hakuna mtanzania aliyenyongwa ikilinganishwa na wachina na wafungwa wa mataifa mengine.
Kumekuwa na habari za kupotosha kwenye baadhi ya vyombo vya habari vya Tanzania kuhusu jambo hili, lakini ukweli ni kuwa Mpaka sasa hakuna mtanzania aliyehukumiwa adhabu ya kifo kwa makosa ya dawa za kulevya na adhabu yake kutekelezwa. Ni vigumu kujua ni kwanini China haijawanyonga watanzania, lakini ukiangalia sababu ya wachina kutowachukulia hatua kali watanzania, utaona kuwa wanathamini sana urafiki uliojengwa na viongozi wetu, hasa mwalimu Nyerere na mzee Salim Ahmed Salim. Kwa hiyo ukiona jinsi wenyeji wanavyochukuliwa hatua kali, na sisi watanzania “kudekezwa”, hata ukikutana na vitendo vinavyokukosesha raha unapopita uwanja wa ndege, basi inabidi uwe mpole mara moja.
Pamoja na kuwa kila suala la dawa za kulevya linapotajwa, utakachoona kwenye vyombo vya habari ni kuwa kuna mtandao mkubwa wa siri, lakini ni kama tunapuuza madhara yanayoletwa na jambo hili kwa uhusiano kati ya nchi yetu na nchi nyingine, na usumbufu linaoleta kwa watanzania wengine wasio wasafirishaji wa dawa za kulevya.
Inasikitisha kuona kuwa kati ya watu kutoka nchi za Afrika Mashariki, ni watanzania ndio wanaokamatwa zaidi na dawa za kulevya kuliko wale wakenya na waganda. Na hata watanzania wanaokamatwa, wengi wanatoka katika Mikoa miwili ya pwani, ambako baadhi ya vijana wanaona ni “ujiko” kusafirisha dawa za kulevya. Ukiongea na vijana hao, unaweza kuona kuwa hawana elimu hata kidogo, kwani hata uwezo wao wa kuandika kwa Kiswahili na uwezo wa kuongea Kiswahili na kujenga hoja ni mdogo sana, ndio maana inaonekana ni rahisi kwao kurubuniwa kuliko vijana wa Kenya, Uganda na wa nchi nyingine za Afrika Mashariki. Wengi wao wanasema wanaahidiwa kati ya dola elfu mbili na elfu nne wakifikisha “mzigo” salama. Kwa kweli hizo si pesa nyingi ikilinganishwa na hatari ya kazi yenyewe, na hasa ukizingatia kuwa kwa mtanzania anayejituma kufanya kazi nyumbani, anaweza kupata pesa hizo.
Kwa hapa China, mpaka sasa naweza kusema kwa sasa tatizo limefikia kiwango cha kutia hofu, na hasa kwa Hong Kong na Makau ambako kuna wafungwa zaidi ya 100 wa kitanzania. Tofauti na siku za nyuma, idadi ya wafungwa wa kike inazidi kuongezeka siku hadi siku ambapo kwa sasa kuna wafungwa wa kike zaidi ya 20 katika magereza ya China bara na Hong Kong. Kutokana na hali hiyo nina wasiwasi kuwa huenda ile hadhi ya watanzania kuingia katika miji hiyo bila Visa huenda iko mashakani. Lakini vigumu kwangu kama mwandishi wa habari kujua undani wa tatizo hili. Ninachojua ni kuwa kuna watanzania wengi wako gerezani, kutokana na kukamatwa kwa makosa yanayohusiana na dawa za kulevya.
Niliwahi kumuuliza aliyekuwa balozi wa Tanzania hapa China na balozi wa sasa kuhusu athari ya tatizo hili kwenye uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania, wote walioonesha kukasirishwa na kusikitishwa na jambo hilo, na kusema linatia aibu. Lakini mabalozi hao hawajui ni nani anayewatuma watanzania wanaokamatwa na dawa za kulevya. Waliokamatwa nao hata siku moja hawataji ni nani aliyewatuma, wao ni kama watu waliokula yamini ya kutosema lolote, hata kama wanapewa adhabu ya kifo. Hata hivyo, wafungwa wanaeleza tu kwamba “Kuna mtandao mkubwa ambao unahitaji ushirikiano mkubwa kupambana nao, zinakopelekwa na zinakotoka dawa hizo”.
Hivi karibuni tumesikia alichokifanya Dk Mwakyembe kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, yeye anaona kuwa uwanja unaobeba jina la Mwalimu Nyerere haupaswi kuhusishwa na dawa za kulevya. Alichofanya Dk Mwakyembe pale uwanja wa ndege kwa kweli ni jambo zuri, na kama asingefanya hivyo huenda watanzania tungeendelea kuwa kizani kuhusiana na mambo yanayoweza kuwa yanaendelea katika forodha zetu. Lakini tukiangalia kwa undani tunaweza kuona kuwa, kama uhalifu huo unatokea kwenye uwanja wa ndege unaotakiwa kuwa na usalama mkali, hali ikoje kwenye forodha nyingine mbali na ile ya uwanja wa ndege wa mwalimu Nyerere ambako hakuna kamera za video, ambako Dk Mwakyembe hawezi kwenda kwa ghafla? Kuna Namanga, Holili, Horohoro, Silari, Tunduma nk, hali ya huko ikoje? Dk Mwakyembe anatakiwa kuhakikisha kuwa kilichofanyika katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere kifanyike katika forodha zote. Dk Mwakyembe analia na jina la Mwalimu Nyerere, lakini ni vizuri watanzania wote tukikumbuka kuwa tunatakiwa kulia na jina la nchi yetu, Tanzania.
Kama hali hii ikiendelea inaweza kufika hatua kuwa wanafunzi, wafanyabiashara, wanamichezo, wagonjwa na hata watalii kutoka Tanzania wanaokwenda nje ya nchi, wote watawekwa kwenye kundi la washukiwa wa biashara ya dawa za kulevya.
- See more at: http://www.fikrapevu.com/watanzania-zaidi-ya-100-wako-gerezani-nchini-china-kuhusiana-na

MZEE GURUMO ASTAAFU MUZIKI


Mwanamuziki mkongwe wa bendi ya Msondo Ngoma Mzee Muhidin Gurumo leo amestaafu rasmi kazi ya muzika alioifanya kwa muda wa miaka 53.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mzee  Gurumo mwenye umri wa miaka 73 amesema ameamua kustaafu kazi hiyo kwa hiari yake mwenyewe kutokana na umri wake kuwa mkubwa.

Mzee Gurumo amesema “Muziki kwangu umekuwa kama asili yangu na kazi yangu lakini nimeamua kustaafu kutokana na umri wangu na nitabaki kuwa mshauri tu kwa mwanamuziki yeyote atakayetaka ushauri wangu”.

Pamoja na kufanya kazi ya muziki Gurumo amesema kuwa hakupata mafanikio makubwa zaidi ya kujenga nyumba anayoishi na familia yake.

Amesema ameimba kwa muda mrefu sana lakini hata baiskeli hana, hata hivyo Mzee Gurumo akasema anashukuru kuwa ana nyumba ya kuishi na familia.

MWIGULU NCHEMBA TENA


MBUNGE wa Iramba Magharibi na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Mwigulu Lameck Nchemba amenaswa tena, safari hii akimlisha chakula mtoto wake mchanga akiwa kitandani ‘on bed’.

Katika picha hiyo iliyonaswa hivi karibuni mtandaoni imemuonesha mbunge huyo akiwa hotelini ikiwa imetupiwa maneno: “Malezi kusaidiana.”

Ilidaiwa kuwa ‘sosi’ ya kusambaa kwa picha hiyo ni yeye mwenyewe ambaye aliitupia kwenye ukurasa wake katika mtandao wa kijamii wa Facebook ambapo ilipata maoni mengi ya wadau waliokuwa wakimsifia na wengine kuitilia shaka kuwa ni usanii.
Kuonesha kuwa anayajua malezi, Mwigulu alikuwa ametenga pampasi pembeni kwa ajili ya kumbadilishia mwanaye kwani watoto wachanga hujisaidia mara kwa mara huku akiendelea kumlisha uji kwa kijiko.

Wadau hao wa mheshimiwa huyo mtandaoni wapatao 306 waliipenda ‘like’ picha hiyo wakimpongeza kwa uamuzi wake wa kusaidiana na mwenzi wake katika kulea mtoto.
Mwezi uliopita, mbunge huyo alianikwa mtandaoni akiwa na familia yake, mke na watoto watu huku akiwa amembeba mmoja mgongoni na kuibua gumzo kubwa.

HITILAFU KATIKA MITAMBO YA KUZALISHA UMEME YA SONGAS JIJINI DAR


HABARI zilizotufikia leo alfajiri ni kwamba palitokea hitilafu katika mitambo ya gesi inayozalisha umeme ya Songas iliyopo Ubungo hali iliyopelekea umeme kukatika jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa mmoja wa mashuhuda aliyekuwepo jirani na eneo la tukio majira ya saa 11 alfajiri, alidai kuwa kulikuwa na moshi mkubwa uliokuwa unatoka eneo hilo hali iliyopelekea wananchi waliokuwa jirani kukimbia huku wakijifunika usoni maana moshi huo ulikuwa unawasha. "Ilikuwa ni vigumu kumuona mtu wa mbele yako kwa wakati huo maana moshi ulikuwa mkubwa" alisema shuhuda huyo. Kwa sasa hali ni shwari eneo hilo baada ya jitihada za zimamoto japo maeneo mengi ya mji bado umeme haujarudi.

“I Have a Dream” 50th Anniversary


50 years ago, Dr. Martin Luther King, Jr. shared his dream in a speech that changed the world. On August 26 at 01:00PM EAT, join a special online film screening of “The March”, a documentary about the 1963 civil rights March on Washington. Celebrate this historic event and chat with civil rights experts at our global viewing party! Learn more at: http://goo.gl/u34BPC 

Wednesday 21 August 2013

FEZA ATUA BOTSWANA











Mahakama yaamuru Mubarak achiliwa

Mahakama mjini Cairo imetoa amri ya kuachiliwa huru kwa aliyekuwa rais wa Misri Honsi Mubarak.
Mahakama hiyo imeamuru Mubarak kuachiliwa huru kutokana na mashitaka ya rushwa yaliyokuwa yanamkabili.Lakini bado haijajulikana kama ataachiliwa baadaye jumatano ya leo.
Upande wa mashitaka unatarajiwa kukata rufaa.
Kiongozi huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 85 anakabiliwa pia na kesi ya kushiriki kwenye mauwaji ya malefu ya raia walioandamana kwenye vuguvugu la mapinduzi lililomtoa madarakani mwaka 2011.
Alifungwa kifungo cha maisha jela mwaka jana, lakini alikata rufaa na kushinda na kesi yake kutakiwa kusikilizwa upya.

Silaha za sumu zawaua mamia Syria

Maiti za raia waliouawa SyriaMamia ya raia wameuawa kufuatia shambulio lililotumia silaha za kemikali viungani mwa Mji Mkuu wa Syria, Damascus. Makundi ya upinzani yanasema makombora yaliyokua na kemikali ya sumu yalilenga eneo la Ghouta usiku wa kuamia Jumatano.
Inadaiwa majeshi ya serikali yalikua yakiwashambulia waasi.Hata hivyo Shirika la utangazaji la serikali limetaja taarifa hizo kama upuzi mtupu,na kusema ni kisingizio tu cha kuwachochea wakaguzi wa Umoja wa Mataifa walioko Syria.
Muungano wa upinzani umesema zaidi ya watu 650 waliuawa katika shambulizi hilo.Makundi mengine ya kiraia pia yametangaza vifo vya mamia katika shambulio hilo japo taarifa hizo hazijathibitishwa kirasmi.
Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague, ametaka utawala wa Syria kukubalia wakaguzi wa Umoja wa Mataifa katika eneo hilo na kusema Uingereza itawasilisha hoja katika Umoja wa Mataifa.
Muungano wa nchi za Kiarabu pia umeunga mkono wakaguzi hao kuingia eneo hilo.Shambulizi hilo ni moja wapo ya operesheni kali ya jeshi la serikali katika maeneo yanayothibitiwa na waasi mjini Damascus.
Maeneo yaliyoathirika na shambulio la karibuni ni pamoja na Irbin,Duma na Muadhamiya.

Mwanasiasa wa Sweden ajeruhiwa Somalia

Watu waliokua na silaha wamewaua watu wawili na kumjeruhi mwanasiasa wa Sweden Ann-Margarethe Livh baada ya kushambulia gari lake mjini Mogadishu, Somalia.
Ann-Margarethe LivhMaafisa wanasema watatu hao walishambuliwa wakati wakirejea katika hoteli ya mwanasiasa huyo baada ya kutoa hotuba kuhusu demokrasia katika chuo kikuu mjini humo.
Hakuna kundi lililodai kutekeleza shambulio hilo wala sababu za kumlenga Bi Livh. Somalia inakabiliwa na maasi ya wanamgambo wa kiisilamu wa Al Shabaab ambapo pia inakumbwa na visa vya jinai.
Wiki jana shirika la misaada la Medecins Sans Frontier{MSF} lilitangaza kufunga huduma zake zote nchini Somalia kutokana na mashambulio dhidi ya wafanyikazi wake.
Somalia imekua bila serikali thabiti tangu kuondolewa madarakani kwa utawala wa Siad Barre mwaka wa 1991.
Duru za usalama zimesema Bi Livh amepokea matibabu katika hospitali ya wanajeshi wa Muungano wa Afrika mjini Mogadishu. Msemaji wa chama cha Ann-Mararethe Livh amesema mwanasiasa huyo alipata majeraha ya risasi.
Kwa sasa kuna mipango ya kumsafirisha hadi mjini Nairobi, Kenya kwa matibabu zaidi.Familia yake imesema mwanasiasa huyo alikua shwari licha ya majeraha.
Takriban wanajeshi 18,000 wa Muungano wa Afrika wanashika doria nchini Somalia ili kusaidia serikali mpya ya Somalia. Utawala wa sasa ndio wa kwanza kutambuliwa na Umoja wa Mataifa, Marekani na Shirika la Fedha duniani kwa zaidi ya miongo miwili.
Wapiganaji wa Al Shabaab wameondolewa mjini Mogadishu lakini wanathibiti maeneo kadhaa ya Somalia. Kuna makundi mengine ya kikoo ambayo yanathibiti maeneo mengi ya Somalia.

Chelsea yapata ushindi wenye utata.


Bao la kipindi cha pili lililofungwa na Branislav Ivanovic kwa kichwa ndilo lililoamua hatima ya Chelsea jumatano usiku kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Stamford Bridge.

Chelsea walianza kwa kufunga kwa shuti la Eden Hazard ambalo lilisindikizwa golini na Antonio Luna wakati akijaribu kuokoa.Lakini Christian Benteke aliisawazishia Villa kwa bao zuri.
Licha ya ushindi huo kwa Chelsea mechi hiyo iligubikwa na utata kutokana na maamuzi ya mwamuzi wa kati Kevin Friend.
Tukio kubwa ambalo limetawala na kuibua utata ni pale beki wa Chelsea Ivanovic alipopewa kadi ya njano kwa kosa la kumpiga au kutishia kumpiga usoni mshambuliaji wa Villa, Christian Benteke.
Kitendo hicho kimesemwa kuwa kilistahili kadi nyekundu badala ya njano aliyopewa Ivanovic, japo kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema kadi hiyo ya njano ilikuwa ni adhabu tosha kwa mchezaji wake.
Kocha wa Aston Villa Paul Lambert ameilalamikia maamuzi ya mechi hiyo ikiwemo pia penati ambayo walinyimwa Villa baada ya John Terry kuushika mpira kwenye eneo la hatari.
Hata hivyo Mourinho amekiri haikuwa mechi rahisi kwake, na kusema "hiki ndicho nimekuwa nikikosa nilipokuwa Hispania,pale kila mechi tunashinda tukiwa nyumbani bila wasiwasi wowote,lakini hapa England mambo ni magumu,uwe nyumbani au ugenini."
Mourinho hajawahi kufungwa kwenye uwanja wa Stamford Bridge,kwani ana rekodi ya kushinda michezo 48 na kutoka sare 14 katika michezo 68 aliyoingoza Chelsea tangu alipofika mara ya kwanza.
Jumatatu Mourinho atakuwa na kibarua kigumu mbele ya Manchester United kwenye uwanja wa Old Traford, kabla ya kwenda kupambana na Bayern Munich katika mechi ya kombe la mabingwa wa Ulaya maarufu kama Super Cup.

Arsenal yaichapa Fenerbahce 3-0


Walipua mizinga wa Kaskazini mwa London, Arsenal wamejiweka kwenye nafasi nzuri ya kushiriki michuano ya klabu bingwa ulaya hatua ya makundi.

Arsenal iliyokuwa ugenini huko nchini Uturuki imeichapa Fenerbahce nyumbani kwao 3-0 katika mchezo ambao ulishuudia kipindi cha kwanza kikimalizika bila Pasi nzuri kutoka kwa Aron Ramsey iliyomkuta Theo Walcott ambaye bila kusita naye aliunganisha hadi kwa Kieran Gibbs aliyelitazama lango la Fenerbahce na kuandika bao la kwanza kwa Arsenal kunako dakika ya 51 ya mchezo.
Dakika chache baadaye Arsenal waliendelea kulisakama lango la Fenerbahce, lakini Aron Ramsey aliongeza matumaini ya kutopoteza mchezo wa pili na kuwapa raha mashabiki wa Ashburton Grove kwa kufunga bao la pili.
Pengine bao la pili liliwachanganya zaidi Fenerbahce ambao licha ya kucheza mechi hiyo bado wapo kwenye adhabu ya kutoshiriki michuano yoyote ya ulaya lakini rufaa waliyoikata ambayo itasikilizwa tarehe 28 mwezi wa Agosti inawafanya waruhusiwe kuendelea na mashindano.
Kinda mwiingereza Theo Walcott alikuwa mwiba kwa Fenerbahce, kwani kunako dakika ya 75 alifanyiwa madhambi ndani ya eneo la kumi na nane na mwamuzi wa kati aliamuru ipigwe penati ambayo mfaransa Olivier Giroud aliipiga na kuandika bao la tatu na la mwisho kwa Arsenal.
Matoke ya mechi nyingine za kufuzu klabu bingwa ulaya, Dinamo Zagreb ilikubali kichapo cha bao 0 - 2 nyumbani kutoka kwa Austria Wien.
Ludogorets nayo ikatandikwa 2 - 4 na FC Basel ya Uswis, wakati Steaua BucureĹźti ilitoshana nguvu na ya 1 - 1 na Legia Warszawa na Schalke 04 ya ujerumani nayo ikashindwa kutamba nyumbani baada ya kutoka sare tasa ya 1 - 1 PAOK.
Arsenal wameshiriki michuano ya klabu bingwa ulaya kwa miaka 14 mfululizo bila kukosa.
Michezo ya marudaniano itapigwa tarehe 27 Agosti. za timu zote kuguswa.
KLABU ya Yanga, kati ya leo na kesho inatarajiwa kukata rufaa kupinga adhabu aliyopewa mshambuliaji wake, Mrisho Ngasa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Wiki iliyopita, kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake, Alex Mgongolwa, ilimwadhibu Ngasa, kifungo cha mechi sita na kulipa sh milioni 45 kwa klabu ya Simba, kutokana na kusaini mkataba kabla ya kwenda Yanga.
Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako, alisema jana kuwa wanatarajia kuwasilisha pingamizi TFF, ambayo itakuwa na mambo matatu muhimu, kwani barua waliyoipata kutoka Shirikisho hilo haijaeleza kwa undani mambo hayo.
Mwalusako alisema, kwanza, watahoji endapo kamati imebariki Ngasa ni halali Yanga, iweje wamfungie mechi sita? Pili, barua waliyopewa haina sehemu inayoonesha mchezaji huyo alisajiliwa na Simba na tatu, haijaonesha vipengele vya kanuni vilivyotumika kutoa adhabu hizo.
Kwa mujibu wa Kamati ya Mgongolwa, endapo Ngasa atashindwa kulipa fedha hizo ndani ya mechi sita alizofungiwa, ataendelea kusota benchi hadi atakapotekeleza adhabu hiyo.

Yanga yaburuzwa TFF,NSAJIGWA, MWASIKA WAIKABA KOO

KLABU ya Yanga imeburuzwa kwa mara nyingine Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kutokana na kushindwa kuwalipa nyota wake wawili wa zamani deni la sh milioni 16.
Wachezaji walioishtaki Yanga TFF ni aliyekuwa nahodha wake muda mrefu, Shadrack Nsajigwa ‘Fuso’, ambaye hivi sasa ni Kocha Mkuu wa Lipuli ya Iringa na Stephano Mwasika, aliyeko Ruvu Shooting ya Pwani.
Hii itakuwa si mara ya kwanza Yanga kushtakiwa katika vyombo vya juu vya soka na hata mahakamani, kutokana na kushindwa kuwalipa wachezaji na wafanyakazi wake inaoachana nao.
Baadhi yao ni Mkenya, John Njoroge, Kocha Kostadin Papic, Steven Marashi, Mmalawi Wisdom Ndlovu, aliyekuwa Ofisa Habari, Louis Sendeu na Katibu Mkuu, Celestine Mwesiga.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako, katika kuonekana kujihami na sakata hilo, alikiri kudaiwa deni hilo linalotokana na ada ya usajili na kuwa, waliwaita Fuso na Mwasika ili walizungumze hilo juzi, lakini hawakutokea na wala simu zao za viganjani hazikupatikana.
Mwalusako alisema wamesikia tetesi za wachezaji hao kwenda TFF kuwashtaki, wakati suala hilo liko mezani na mikataba yao inasema mchezaji anaweza kulipwa kidogo kidogo hadi deni lake kumalizika.
“Nimeamua kuwaita hapa kuzungumzia suala moja la Mwasika na Nsajigwa, tumesikia wamekwenda kutushtaki TFF, na sisi tuliwaita ili tuzungumze na kumalizana lakini hawakutokea, tumeona tuwaambie yasije yakafika kwenu mkaandika,” alisema Mwalusako na kuongeza kuwa, Nsajigwa anadai sh milioni 10 na Mwasika sh milioni sita.
Tanzania Daima iliwasaka Mwasika na Nsajigwa kuzungumzia suala hilo ambao walikiri kwenda TFF, baada ya kuona uongozi wa Yanga unawazungusha juu ya madai yao ambayo ni halali, baada ya kumaliza mikataba yao.
Mwasika alisema wao si watoto wadogo hadi waamue kwenda TFF bila sababu muhimu na kuwa kilichosababisha kupiga hodi vyombo vya juu ni ili kupata msaada wa kulipwa fedha zao ambazo walitakiwa kuzipata kabla hata ya kumaliza mikataba yao.
Alikwenda mbali na kudai kuwa, Mwalusako anaudanganya umma, kwani licha ya kutakiwa kuwalipa fedha zao Januari mwaka huu, hajawahi kuwaita kwa ajili ya mazungumzo na hiyo ni kutaka kujitetea.
Alihoji, hivi sasa yeye si mchezaji wa Yanga, yuko Ruvu Shooting, atawezaje kuacha kazi yake na kwenda Yanga kujadili mambo hayo?
“Dada yangu kwanza mimi nakushukuru kwa kunipigia simu, kwa sasa nawaza nifanyeje ndani ya timu yangu ya Ruvu Shooting na mimi nawadai Yanga, wanilipe changu tumalizane, hawajatuita kuzungumza nao kama wanavyodai, kila siku wanatuzungusha, ndiyo maana tumeamua kwenda TFF.
Huyo Mwalusako ni muongo, mimi nadai hela zangu na kama angeniita nikafuate ningekataa saa ngapi? Nawadai sh milioni 6.5 na si sita kama alivyosema,” alisema Mwasika.
Kwa upande wake Nsajigwa, alisema kwa sasa yeye yuko Iringa kikazi, muda wa kukaa na Yanga kuzungumzia stahiki zake hana, kwani cha muhimu sasa ni TFF kuwasaidia kutoa uamuzi na endapo itashindikana, wako tayari kwenda Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).
“Mpaka kufikia hatua hii tumewavumilia sana na sasa tumechoka, ila tuna imani TFF watatusaidia na tunashukuru kama wao Yanga wamekubali kuwa tunawadai, hilo ndilo la msingi na mimi niko ‘bize’ na kazi zangu, siwezi kuacha kazi zangu nikaja Dar es Salaam kujadili mambo ya hela, tumechoka na hatukutaka kufikia hapa ila imebidi, kwani sisi si wachezaji wa kwanza kulalamika,” alisema Nsajigwa.

Chanzo Tanzania Daima

Jairo, Nyoni watupwa

RAIS Jakaya Kikwete amewang’oa rasmi makatibu wakuu wawili waliokuwa wamesimamishwa kazi kutokana na tuhuma za ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi zilizokuwa zikiwakabili katika wizara zao.
Makatibu hao ni David Jairo aliyekuwa Wizara ya Nishati na Madini na Blandina Nyoni wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Viongozi hao walisimamishwa kazi kwa vipindi tofauti mwaka juzi na mwaka jana ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yao.
Jairo alisimamishwa kazi kwa tuhuma za kuandika barua kwa idara mbalimbali za Wizara ya Nishati na Madini na kuchangisha fedha ambazo zingetumika kuwashawishi wabunge wapitishe bajeti ya wizara yake kinyume cha utaratibu.
Nyoni alisimamishwa kazi pamoja na aliyekuwa mganga mkuu wa serikali, Dk. Deogratius Mtasiwa wakati mgomo wa madaktari wakidaiwa kuwa chanzo kutokana na kujihusisha na miradi ya kibishara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Akitangaza mabadiliko hayo ya makatibu wakuu jana Ikulu jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema uteuzi huo unalenga kuboresha utendaji serikalini.
Aliwataja walioteuliwa kuwa makatibu wakuu kwenye wizara nyingine ni Dk. Florence Turuka aliyekuwa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia na sasa anakwenda Ofisi ya Waziri Mkuu.
Joyce Mapunjo kutoka Viwanda, Biashara na Masoko kwenda Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Alphayo Kadata aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Viwanda, Biashara na Masoko anakwenda Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Wakati Shaaban Mwinjaka aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Viwanda, Biashara na Masoko anakwenda Uchukuzi, Uledi Mussa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Ushirikiano wa Afrika Mashariki anakwenda Viwanda, Biashara na Masoko.
Uteuzi huo pia umemgusa aliyekuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) Sifuni Mchome anayekuwa Katibu Mkuu Elimu na Mafunzo ya Ufundi, huku Charles Pallangyo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anakuwa Katibu Mkuu Afya na Ustawi wa Jamii.
Waliopandishwa vyeo kutoka manaibu na kuwa makatibu kamili kwenye wizara hizo hizo ni Jumanne Sagini (Tamisemi), Servacius Likwelile (Fedha na Uchumi) na Patrick Makungu (Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia).
Wengine ni Anna Maembe (Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto), Sihaba Nkinga (Habari, Vijana Utamaduni na Michezo) na Sophia Kaduma (Kilimo Chakula na Ushirika).
Awali Balozi Sefue alisema Rais Kikwete amemteua Dk. Donan Mmbando kuwa Mganga Mkuu wa Serikali akishika nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Mtasiwa aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Tamisemi atakayeshughulikia afya.
Akifafanua sababu za uteuzi wa Dk. Mtasiwa, Balozi Sefue alisema: “Tuhuma zake hazikumfanya rais aamini kwamba anastahili adhabu ndiyo maana amempangia kazi nyingine.”
Kwa upande wa manaibu makatibu wakuu, walioteuliwa na waendako kwenye mabano ni Angelina Madete (Makamu wa Rais Mazingira), Regina Kikuli (Ofisi ya Waziri Mkuu), Zuberi Samataba na Edwin Kiliba (Tamisemi).
Wengine ni Dk. Yamungu Kayandabila (Kilimo, Chakula na Ushirika), Profesa Adolf Mkenda, Dorothy Mwanyika (Fedha na Uchumi), Rose Shellukindo (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa) na Selassie Mayunga (Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi).
Wamo pia Monica Mwamunyange (Uchukuzi), Consolata Mgimba (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Profesa Elisante Ole Gabriel (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo) na Armatius Msole (Ushirikiano wa Afrika Mashariki).
Balozi Sefue aliwataja manaibu makatibu waliohamishwa kuwa ni John Mngodo kutoka Uchukuzi kwenda Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Selestine Gesimba kutoka Elimu na Mafunzo kwenda Maliasili na Utalii.
Uhamisho huo umemgusa pia Injinia Ngosi Mwihgava kutoka Makamu wa Rais kwenda Nishati na Madini, Maria Bilia kutoka Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwenda Viwanda na Biashara wakati Nuru Milao aliyekuwa Maliasili na Utalii akipelekwa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
Watakaopangiwa kazi nyingine ni Sethi Kamuhanda aliyetoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamadini na Michezo, Kijakazi Mtengwa aliyekuwa Jamii, Jinsia na Watoto na Omari Chambo aliyekuwa Uchukuzi wakati Peniel Lyimo aliyekuwa Ofisi ya Waziri Mkuu akihamia Ikulu kama naibu mtendaji mkuu mwenye jukumu la kuanzisha na kuongoza Idara ya Mageuzi ya Kilimo.
Kwa mujibu wa Balozi Sefue, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo ya Makazi Patrick Rutabanzibwa amestaafu kwa hiyari.

Chanzo Tanzania Daima

UTALII ZANZABAR,vijana kujihusisha na ngono nzebe

 















Tunatazama utalii- Vijana wa Zanzibar wanavyojihusisha katika uhusiano wa kimapenzi na watalii wa kike ili kupata fedha na watalii hao pengine kupata raha za kimapenzi. Lakini kuna wasiwasi kuwepo kwa ngono zisizo salama. 

Urais wamtesa Makamba, VYUO VIKUU WAKANA TAMKO LA KUMUUNGA MKONO

NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba amechafua hali ya hewa kwa viongozi wa vyuo vikuu, akidaiwa kuwatumia baadhi yao kujisafishia njia ya urais 2015.
Siri hiyo imefichuka zikiwa ni siku tano tangu Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe tawi la Mbeya, Theonest Theophil atoe taarifa akidai kuwa viongozi wa vyuo vikuu 21 nchini wameazimia kuunda timu ndogo kumshawishi awanie urais.
Katika tamko hilo ambalo limebatilishwa jana na Taasisi ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini (Tahliso), Theophil alisema maazimio hayo yalifikiwa katika mkutano wa siku mbili na  kuwashirikisha marais, makamu wa rais, mawaziri wakuu na maspika wa vyuo 21 nchini.
Theophil alisema mkutano huo uliyapigia kura majina matatu ya wabunge vijana wakiwemo pia John Mnyika na Zitto Kabwe wa CHADEMA, na kwamba Makamba alipitishwa kuwa chaguo lao baada ya kupata kura 70 kati ya 105 zilizopigwa.
Kwamba Zitto alipata kura 20 na Mnyika kura tisa, huku kura tisa zikiharibika.
Hata hivyo, taarifa hiyo iliibua mvutano mkali baina ya viongozi wa vyuo mbalimbali wakisema kuwa semina hiyo haikuwa ya kujadili suala hilo na kwamba hakuna kura zilizopigwa.
Badala yake viongozi hao walidai kuwa taarifa hiyo ya upotoshaji iliandaliwa kwa makusudi na baadhi ya wenzao ambao wamekuwa wakijaribu kuitumia taasisi hiyo kwa malengo ya kumpigia chapuo Makamba ambaye pia ni mbunge wa Bumbuli.
Wakati hali ikiwa hivyo, asasi isiyokuwa ya kiserikali inayojihusisha na mapambano dhidi ya maradhi, ujinga na umasikini (FDIP) ambayo iliitisha semina hiyo mkoani Morogoro, imekuwa na kauli za kugongana na mtoa taarifa za maazimio.
Katibu Mkuu wa FDIP, Francis Nduguru alipobanwa na gazeti hili jana, alidai kuwa aulizwe Theophil ambaye alitoa taarifa ya maazimio hayo ya semina ya siku mbili.
“Sitaki usumbufu, hao viongozi wanakulalamikia wewe kama nani? Waite walalamikie kisha tumia taaluma yako kufanya kile ambacho kinakusaidia, nimemaliza,” alisema Nduguru na kisha kukata simu.
Naye Theophil alipoulizwa alitoa tamko hilo kama nani wakati Tahliso wanalipinga, alirusha mpira akisema “naona vyema ungewauliza waandaji wa semina hiyo.”
Alipoelezwa kuwa nao wamemtaka alifafanue yeye, alikiri kuwa semina hiyo haikuwa ya Tahliso, lakini walikuwa wakijadili changamoto zinazowakabili vijana ikiwemo ya kukosa uwakilishi katika vyombo vya uamuzi.
“Alipoulizwa agenda ya kumchagua Makamba ilitoka wapi, alisema kuwa katika majadiliano jina la mbunge huyo lilitajwa na vijana wengi, lakini akataka waandaaji wa semina hiyo ndio watoe ufafanuzi.
Makamba hakupatikana kuzungumzia madai hayo kutokana na simu yake kuita bila kupokelewa, na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maandishi hakujibu.
Gazeti hili lilifanikiwa kupata nakala ya barua ya mwaliko na ratiba ya semina hiyo ambapo suala la wajumbe kujadili wagombea na kuwapigia kura halikuonyeshwa popote.
Rais wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Katoliki cha Afya na Tiba-Bugando (CUHAS-Bugando) Mwanza ambaye ni mmojawapo wa viongozi wanaopinga taarifa ya Makamba kupigiwa debe na vyuo, alisema kuwa wasomi wa vyuo vikuu hawawezi kufanya jambo ambalo ni kinyume na katiba za serikali zile za vyuo.
“Kiongozi wa serikali kusimama na kutoa tamko la kumuunga mkono mtu ambaye ni mwanachama wa chama fulani cha siasa kwa mujibu wa katiba za serikali zetu haturuhusiwi kwani si za vyama vya siasa,” alisema Moses Mdede.
Nayo Tahliso katika taarifa yake iliyosainiwa na Katibu Mkuu Mtendaji Donati Salla, ilieleza kusikitishwa na maazimio hayo kwa kuwa yalikuwa kinyume na maadili ya elimu ya juu nchini.
“Tahliso inasema mkutano huo wa Morogoro ni batili na hautambuliki kwa mujibu wa sheria Na 7 ya vyuo vikuu ya mwaka 2005,” alisema.
Salla aliongeza kuwa shughuli za wanafunzi wa vyuo vikuu vya elimu ya juu ni kushughulikia masuala ya wanafunzi na ubora wa taaluma itolewayo katika chuo husika na masuala mengineyo ya kitaifa yasiyokuwa ya kisiasa.
“Hatua zilizochukuliwa na Tahliso ni kuwaonya viongozi wa serikali za wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu ambao walishiriki mkutano huo wa Morogoro na kuwataka wasirudie tena kufanya hivyo,” alisema.
Vyanzo vyetu vya habari vinadai kuwa semina hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Uluguru, ilionekana wazi kuwa ilipangwa makusudi kumjenga kisiasa Makamba.
Kwa mujibu wa nyaraka tulizonazo, ajenda zilizojadiliwa ni elimu na mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Katika hili vijana walitakiwa kutoa mawazo yao juu ya mfumo wa elimu nchini kwa ujumla na wachangiaji pia waligusia suala la mikopo ya wanafunzi.
Katika tatizo la ajira nchini hasa kwa vijana ambao wengi wao ni wahitimu wa vyuo vikuu, mada hii nayo ilijadiliwa kwa wachokoza mada na wajumbe kujadili na kutoka na mapendekezo.
Kuhusu vijana na siasa, ajenda hii ilijikita katika mrengo wa namna gani vijana wataweza kuhusika katika siasa ya nchi hasa katika chaguzi zijazo kuanzia serikali za mitaa mwaka 2014 na uchaguzi mkuu mwaka 2015.
“Kilichoonekana katika semina ile ni kwamba viongozi wa vyuo vikuu waliohudhuria walikuwa ni wachache sana na hawakufika idadi hiyo iliyotajwa na vyombo vya habari.
“Wajumbe wengi waliohudhuria walionekana ni watu waliokuwa wameandaliwa maalumu kwa ajili ya kazi fulani kwani kuna ambao walionekana hata hawakuwa wanachuo,” kilisema chanzo hicho.
Katika hatua ya kushangaza wakati semina inaanza mwenyekiti alikuwa tayari ameshaandaliwa kinyume cha utaratibu kwani mwenyekiti hupendekezwa na kuchaguliwa na wajumbe.
“Pia mfumo wa kujadili mada zilizochokozwa ulikuwa ni wa makundi. Katika kila kundi ilionekana kulikuwa na mamluki waliowekwa ili kufanikisha mpango huo.”
“Ilipofika katika mada ya vijana na siasa, kwenye kila kundi ilionekana kulikuwa na mtu aliyetaka wajumbe watoke na pendekezo la kumtaja Makamba kuwa ndiye awe mgombea urais 2015,” alisema.
Ratiba ilionyesha kuwa baada ya chakula cha mchana kulikuwa na muda wa wajumbe mmoja mmoja kutoa mawazo yake kwa mada zilizojadiliwa.
Hata hivyo, waandaaji walipoona wajumbe wanataka kuhoji jina la Makamba kutajwa ndani ya ukumbi kinyume cha mada zilivyoelekeza, walikiondoa kipengele hicho na baada ya chakula semina ilifungwa.
Lakini hadi wajumbe wanatoka ukumbini hakuna kura yoyote iliyopigwa kumpendekeza yeyote kuwa mgombea urais na wala hakuwepo mwandishi yeyote wa habari.
Viongozi hao wa vyuo wanadai kuwa Makamba amekuwa akijipenyeza katika Tahliso kwa kutumia baadhi viongozi, wakitolea mfano kongamano la Baraza la Katiba la taasisi hiyo liliofanyika Mzumbe tawi la Mbeya Agosti 2 na 3, mwaka huu.
Kwamba Tahliso baada ya kongamano walitakiwa watoe mapendekezo yao kuhusu rasimu ya katiba mpya, lakini Makamba anadaiwa kufika mkoani humo usiku na kukutana na baadhi ya wajumbe.
Katika mazungumzo na wapambe wake, inaelezwa kuwa alitaka wapenyeze suala la umri wa mgombea urais katika tamko la mapendekezo yao kwamba miaka iwe kuanzia kati ya 30 na 35 ili kumpa yeye nafasi ya kutimiza azma yake.
Mkakati huo unadaiwa kuratibiwa na kijana mmoja anayetajwa kwa jina la Tibaigana ambaye alihudhuria kongamano la Mbeya na semina ya Morogoro akijitambulisha kama mkurugenzi wa FDIP.
Katika semina ya Morogoro wajumbe walilipwa nauli kati ya sh 14,000 hadi sh 100,000 kwa kwenda na kurudi walikotoka pamoja na posho ya chakula na malazi sh 70,000 kila mmoja.

Chanzo Tanzania Daima

SIRI NZITO ZA RWANDA KUCHOKOCHOA TANZANIA.. ZAFICHUKA.hizi hapa

Historia ya Rwanda ni ndefu iliyojaa misukosuko ya kisiasa, kupinduana, vita na mauaji ya wenyewe kwa wenye yaliyosababishwa na ubaguzi wa kikabila.
 
Rwanda imekuwa ikipita katika vipindi vigumu na vya hatari. Vipindi hivi hufuatana na mauaji ya raia wa nchi hiyo, sio tu kutokana na sababu za ukabila bali pia uongozi mbaya wa kisiasa.
 
Mwaka 1959, mtawala wa Kitutsi aliyekuwa akiitawala nchi hiyo na kulalamikiwa kuwa utawala wake ulikuwa ukiwaneemesha zaidi Watutsi walio wachache, uliangushwa na Wanyarwanda wa Kabila la Kihutu.
 
Mabadiliko haya yalifuatiwa na mauaji ya takriban Watutsi 150,000. Walioponea chupuchupu walikimbilia nchi mbalimbali jirani na Rwanda. 
  
Ni wakati huu wazazi wa Rais wa sasa wa Rwanda, Paul Kagame walikimbilia nchi jirani, Uganda yeye akiwa na umri wa miaka miwili.

Baada ya hapo, Wahutu wakaunda Chama cha PARMEHUTU, kikiongozwa na Gregoire Kayibanda, ambaye baadaye alikuwa Rais wa Rwanda.
 
Mtu angedhani wakati huo kuwa kwa sababu uongozi wa nchi hiyo ulichukuliwa na kudhibitiwa na mtu kutoka kabila la Wahutu waliokuwa asilimia 88 ya Wanyarwanda wakati ule, (Watutsi wakiwa asilimia 11 na asilimia moja Watwa), kusingekuwa na chokochoko tena. Utawala ungekuwa wa amani, wapi?
 
Mapinduzi ya kijeshi
Kinyume na matarajio, Julai 5, 1973 Serikali hii nayo ilipinduliwa. Mapinduzi haya yalifanywa na jeshi la Wahutu wakiongozwa na Meja Jenerali Juvenal Habyarimana, ambaye naye alikuwa Mhutu.
 
Cha ajabu, licha ya tofauti hizo za kikabila, mapinduzi hayo yalifanywa na Wahutu walio wengi wakishirikiana na Watutsi wachache. Hii ilitokana na malalamiko kuwa Rais Kayibanda alikuwa akiendesha nchi kama familia yake, akipitisha uamuzi bila kushirikiana na viongozi wengine.
 
Baada ya mapinduzi hayo, kiongozi huyo mpya alibadilisha mambo mengi ikiwa ni pamoja na kusambaratisha chama kilichokuwa kikiongozwa na Kayibanda, PARMEHUTU, badala yake akaunda Chama cha National Revolutionary Movement for Development MRND.
 
Miaka takriban 17 baadaye kutokana na kile kilichoonekana kama utawala wa kikandamizaji, Watutsi waliokuwa nje ya nchi walishirikiana na Wahutu wa ndani kuanza harakati za kuiangusha Serikali ya Habyarimana.
 
 
Harakati hizi ndizo zilizomwingiza madarakani Rais wa sasa, Paul Kagame. Malalamiko kama yale yaliyosababisha mapinduzi dhidi ya mtangulizi wa Habyarimana yakajitokeza tena.
Mtu anayeangalia na kuchambua hali ya mambo ilivyo hivi sasa hachelewi kung’amua kuwa hali kama ile iliyozikumba tawala za tangu utawala wa kifalme wa Watutsi na tawala za Kihutu zinajitokeza tena.
 
Na hii inaifanya hali iwe tete kuliko wakati wowote. Wengi wanaamini kama yatatokea mapigano au mabadiliko katika Serikali ya Kigali pengine hali inaweza kuwa mbaya kuliko ilivyowahi kushuhudiwa.
 
Hivi sasa Wanyarwanda hasa kutoka Kabila la Kitutsi na ambao walikuwa bega kwa bega na Rais Kagame, baadhi ya wasomi na maofisa wa juu kutoka jeshi la RPF wameikimbia Rwanda na tayari kuna kampeni za chini kwa chini kutoka makabila yote mawili kuupinga utawala wa Kagame.
 
Mbaya zaidi kuna kundi kubwa la vijana waliozaliwa baada ya mauaji ya Rwanda. Hili ni kundi kubwa na mtu yeyote ambaye amekuwa akitembelea kambi za wakimbizi kwa miaka mingi anaelewa ninachoelezea hapa.
 
Mwaka 1997 nikiwa na waandishi wenzangu tulitembelea kambi za wakimbizi kutoka Rwanda. Kulikuwa na idadi kubwa ya watoto. Mmoja wetu alimuuliza mmoja wa wakimbizi kwa utani “nyinyi mpo kwenye matatizo mbona mnazaa watoto wengi hivi, hamuoni ikiwa mnajiongezea mizigo”?
 “Hawa ndio watakuja kuikomboa Rwanda,” alijibu kiongozi wa wakimbizi huku akipigiwa makofi na kundi la vijana waliokuwa pembeni kusikiliza mahojiano, katika kambi ya Mbuba wilayani.
 
Nadharia hii imekuwa ikiendelea kwa miaka mingi. Hata tulipotembelea kambi nyingine tukiandamana na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia wakimbizi Ulimwenguni (UNHCR), Antonio Guateres karibu waandishi wengi hawakuficha hisia zao za kushangazwa na kasi ya kuzaana katika kambi za wakimbizi.
 
Fikiria kwa utaratibu huu watoto waliozaliwa tangu mwaka 1994 ni watu wazima. Kama ni wanajeshi ni jeshi kubwa tena lenye hamasa kubwa ya kurudi katika nchi yao Rwanda katika wakati ambapo wanaona kikwazo ni Kagame na Serikali yake.
 
Hivi Kagame anajua kuwa kundi hili halibanwi na tuhuma za mauaji ya halaiki ya Rwanda ya mwaka 1994?  Hata wale wanaotafutwa sio tena kitisho dhidi ya Serikali ya Kigali sababu ni wazee sasa, wa kuogopa ni jeshi hili kubwa la vijana. 
 
Hawa Kagame anawabana na sheria gani? Isipokuwa kwamba wanajiandaa kupigana na Serikali yake kama yeye alivyofanya kuipindua Serikali ya Habyarimana akitokea Uganda?
 
Kibaya zaidi ni kuwa makundi haya katika ukanda wa Maziwa Makuu, wana mawasiliano na kwa nyakati fulani yanasaidiana.
 
Ushauri wa Rais Kikwete
Ninaamini hiki ndicho kilichomsukuma Rais Kikwete kutoa ushauri kwa marais hawa majirani zetu kuwa wasifanye kosa wazungumze na waasi. Heri kupatana nao kwa sasa kuliko baadaye wakisharidhika kuwa wamejiandaa vizuri na wakaanza mapigano rasmi.
 
Kila mwenye macho ya kuona mbali hachelewi kumshauri Kagame chonde chonde ongea na waasi hawa, badala ya kujiridhisha kuwa ni watuhumiwa wa mauaji ya halaiki, wakati wengine mauaji hayo yalitokea wakiwa na umri wa miaka sita na kurudi chini, hawa ni jeshi kubwa lenye uwezo wa muda mrefu wa kukaa msituni, ni hatari.
 
Yapo maswali kadhaa ya kujiuliza, hivi kwa nini Rais Kagame hakioni hiki tunachokiona sisi? Kwa nini hakioni hiki ambacho amekiona Rais mwenzake Kikwete?
 
Ninaamini Rais Kikwete hakukurupuka, ana vyombo vya kiintelijensia vinavyomfahamisha kinachoendelea sio tu Tanzania, lakini hata katika mapori makubwa na Misitu ya DRC.
 
Kagame anapaswa kusoma alama za nyakati, asikimbilie kusema “watuache Rwanda tumalize matatizo yetu,” kwani baada ya mauaji ya mwaka 1994 nchi hiyo ililaumu jumuia ya kimataifakuwa  haikuisaidia Rwanda kuepuka mauaji hayo.
Kama walivyosema Wahaya kuwa “ajuna akanyonyi ajuna akakyahalala” maana ukitaka kumsaidia ndege msaidie akiwa bado ana uwezo wake wa kupaa.
 
Badala yake ametoa lugha za matusi kashfa hadi kutoa vitisho dhidi ya Tanzania, ati kwa ushauri aliopewa na Rais Kikwete, kuwa azungumze na waasi wa Democratic Forces for The Liberation of Rwanda (FDLR).
 
Kikwete alitoa ushauri huo kwenye Kamisheni ya Ulinzi na Usalama ya Umoja wa Afrika wakati wa Mkutano wa wakuu wa nchi za umoja huo uliofanyika mwanzoni mwa Juni mwaka huu, mjini Addis Ababa, nchini Ethiopia.
 
Ushauri huo umegeuka mwiba na kitanzi dhidi ya uhusiano uliokuwepo kati ya Tanzania na Rwanda, ingawa wengine tunajua uhusiano huo haukuwa barabara tangu awali kwani kiongozi huyo wa Rwanda mara kwa mara amekuwa akiisimanga Tanzania hata kabla ya ushauri huo kutolewa. 


Imekuwa kama vile jirani yetu huyu amepata turufu muhimu ya kuitishia Tanzania.
 
Kinachoshuhudiwa sasa ni vita ya maneno baina ya nchi hizi mbili yaani Tanzania na Rwanda.Vita ya maneno na majibizano ya namna hii mataifa hujikuta katika vita kamili.
 
Kwa upande mwingine wengi walishangaa kwa nini Kagame aonekane kukerwa sana wakati ushauri huo haukumhusu yeye peke yake?
 
Wakati Paul Kagame akikabiliwa na kundi linaloinyemelea nchi yake la FDLR, Joseph Kabila, wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anapambana na waasi wa sasa wa M23,  na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda akitishiwa na makundi mawili.  Allied Democratic Force (ADF) na Lord’s Resistance Army (LRA).


Hata hivyo, si Tanzania pekee ambayo imeona hatari inayoinyemelea Rwanda bali hata moja ya makanisa nchini Rwanda.
Kanisa hilo lilipeleka ujumbe hivi majuzi hadi Ikulu ya Kagame likitabiri kuwa Rwanda inakabiliwa na matatizo makubwa na kuwa inaweza tena kudidimia katika mgogoro mkubwa. Watumishi hao wa Mungu wameishia kukamatwa na kuambiwa wanataka kuvuruga amani kuleta mgororo wa kikabila.
 
Uasi zaidi
Kila kukicha wanajeshi wa Rwanda wanazidi kulikimbia jeshi lao na nchi yao, siku zilizopita walikuwa wakikimbilia Uganda siku hizi baada ya kuzidishwa ulinzi katika mpaka wa nchi hizo mbili sasa wanakimbilia Afrika Kusini, nchi ambayo inajua kwa hakika kitu gani kinaendelea nchini Rwanda. Inawapa hifadhi ya ukimbizi wa kisiasa.
 
Miongoni mwao ni aliyekuwa Mkuu wa Usalama katika Jeshi la RPF, Luteni Jenerali Faustin Kayumba Nyamwasa. Huyu alianza kutofautiana mapema na Kagame, baadaye akamsogeza mbali na nchi hiyo. Akamteua kuwa Balozi wa Rwanda nchini India.
 
Bado Kagame aliendelea kumwona ofisa huyo tishio, hivyo akamtuhumu kuwa alihusika na milipuko ya mabomu February 2010 mjini Kigali.  Wakati Kagame akiandaa utaratibu wa kumkamata habari zikavuja, ofisa huyo akatoroka kutoka India hadi Afrika Kusini anapoishi sasa.
 
Inafahamika kuwa maofisa wenye uwezo kama wa Nyamwasa wakipata ushirikiano na wanamgambo wa Kihutu walio sehemu mbalimbali nje ya Rwanda ni rahisi kuishambulia Rwanda, ndio maana inasemekana wametumwa makachero kumuua Nyamwasa kule kule Afrika Kusini lakini ‘wakachemka’ na kuishia kwenye mikono ya polisi ambapo walikiri kutumwa na Serikali ya Kigali, kumuua Nyamwasa.
 
Mwezi Juni 2010, Kiongozi wa Timu ya mpira wa miguu wa Rwanda Brigedia Jenerali Jean Bosco Kazura, alikwenda Afrika Kusini kuangalia mashindano ya kombe la dunia, lakini aliporejea Rwanda akakamatwa kwa tuhuma kuwa akiwa huko alifanya mawasiliano na Nyamwasa na kwa maana hiyo akaingizwa katika kundi la wanaotaka kuiangusha Serikali ya Kagame.
 
Jean-LĂ©onard Rugambage, mwandishi wa habari ameuawa na makachero ikisemekana kuwa alikuwa akitumiwa na Nyamwasa.


Maofisa wa Serikali ya Rwanda wanapotetea msimamo wa Rais Kagame wa kuikejeli Tanzania wanadai kilichomkasirisha bosi wao ni kushauriwa akae meza moja na wale anaowaona kama wauaji wa halaiki wa mwaka 1994, na kuwa ushauri huo ni sawa na kucheza juu ya makaburi ya Wanyarwanda waliopoteza maisha katika mauaji hayo.
 
Hata kama ingekuwa hivyo, basi angewachukia waasi wale lakini sio Tanzania kwa sababu baada ya mauaji ya Rwanda, iwe Kagame au waasi wenyewe hakuna upande wowote uliowahi kuituhumu Tanzania kuhusika kwa namna yoyote katika mauaji hayo, kwa sababu wanajua kuwa nchi hii ilikuwa ikijua kila kilichokuwa kikiendelea na kikifanywa na kila upande kabla na baada ya mauaji hayo.
 
Na hapo ndipo lilipo ‘fumbo la imani’ kwa nini Kagame amechukia sana kwa ushauri ule.
 
Sababu nyuma ya pazia
Udhaifu wa sababu ya chuki za Kagame unaashiria  kwamba kilichoikasirisha Rwanda ni uamuzi wa Tanzania kupeleka jeshi lake lishiriki kulinda amani DRC, na sio ushauri ule.
Alijua kuwa sasa mengi  yatafumuka, ambayo tayari Tanzania inayafahamu ikichanganya na yale itakayoyagundua DRC. 

Nina mifano mingi na ushahidi wa kimazingira hebu nitaje mmoja na kumalizia makala yangu.
 
Yaliyotokea 1994
Rwanda inajua, Kagame anajua, na dunia nzima inajua kuwa mauaji ya kimbali ya Rwanda yalikolezwa zaidi ya kutunguliwa ndege ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo wakati huo, Habyarimana.
 
Habyarimana na mwenzake wa Burundi, Syprian Ntaryamirwa walikuwa wakitoka Arusha nchini Tanzania katika mojawapo ya mikutano yenye lengo la kuangalia namna ya kugawana madaraka baina ya Serikali ya Kigali ya wakati ule na kundi la waasi siku zile RPF.
 
Kikundi hiki cha RPF kikiwa na Watutsi wengi kilikuwa kimeanzisha mapigano dhidi ya Serikali ya Habyarimana miaka miwili kabla wakipigana kutokea nchini Uganda wakitaka Serikali itoe nafasi  kwa Watutsi karibu lakini tano waliokuwa wakiishi nje ya Rwanda.
 
Licha ya Serikali ya Habyarimana kusaini makubaliano ya kuwaingiza waasi wa RPF katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa, Wahutu ambao ndio walio wengi walikuwa hawakubaliani na jambo hili.Kwa hiyo, fikiria inakuja kufahamika kuwa Watutsi wale walioanzisha mashambulizi kutokea nchini Uganda, wametungua ndege ya Rais wa kabila lao na kumuua pamoja na makamanda wa ngazi za juu wa jeshi la Rwanda la wakati ule.
 
Ndio maana baada ya kutunguliwa ndege hiyo Aprili 1994 mauaji ya kutisha yaliyodumu kwa siku mia moja yaliendelea na kugharimu maisha ya Wanyarwanda laki  nane, wengi wao wakiwa Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani.

-Imeandikwa  na  Christopher Buke   wa  gazeti  la  mwananchi.