Wednesday 16 April 2014

Wanaume Vifua wazi marufuku Uingereza.


Wanaume wanaovua mashati wamepigwa marufuku kuitembelea bustani ya mapumziko na kujivinjari ya Adventure Island.
Ni eneo ambalo watu wanakwenda kujivinjari na familia zao, kwa kutazama wanyama, watoto hupata kubembea na pia watu huota jua.Bustani hiyo iliyopo mjini Southend nchini Uingereza, imeweka ilani zinazowaomba wanaume wasivue mashati yao, na kwamba watakao patikana watafukuzwa.
Mkurugenzi mkuu, Marc Miller, amesema anataka wanaume waonyeshe "ustaarabu".

No comments:

Post a Comment