Friday 28 February 2014

Kurasa za mwanzo na mwisho magazetini leo February 28 2014

.
.
Ni utaratibu wa millardayo.com kila siku kukupa nafasi ya kusoma kurasa za mwanzo na mwisho za magazeti mbalimbali ya Tanzania.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Ex-girlfriend wa Samuel Eto’o ashtua watu kuhusu umri wa mchezaji huyo.

hu
“Tatizo la Chelsea ni kukosa wafungaji, nina Eto’o ambaye ana miaka 32 au labda 35 nani anayejua?”.
Hiyo ilikua ni kauli ya kocha Jose Mourinho akimzungumzia Samuel Etoo na baadae mpenzi wa zamani wa Eto’o aliongea kuhusu umri wa mchezaji huyo kitu ambacho kimewashangaza watu wengi.
Anna Barranca alikuwa mpenzi wa zamani wa Eto’o na kupata mtoto mmoja wa kike ambaye hivi sasa ana miaka 11 amesema Eto’o ana miaka 39 kuelekea 40 na sio 35.
Mwanamke huyo amesema kwamba alijua kuhusu umri wa Eto’o wakati wapo Cameroon kutoka kwa mtu ambaye alikua pamoja na Etoo tangu utotoni.

Tuesday 25 February 2014

James Mapalala:Mwanzilishi wa mageuzi aliyeishia kwenye mikosi.

HARAKATI za mageuzi nchini zina historia ndefu, zikianza kabla ya uhuru ambapo wa wananchi kupitia vyama na vuguvugu za aina mbalimbali waliungana ili kuwaondoa wakoloni.
Hadi mwaka 1961 chama cha Tanu kilichokuwa kikiongozwa na Mwalimu Julius Nyerere kilishinda uchaguzi na kuunda Serikali.
Vyama vingine vilivyokuwepo ni pamoja na AMNUT, ANC na UTP.
Baada ya Mwalimu kuunda Serikali, alifanya mabadiliko kadhaa ambapo mwaka 1965 alifuta mfumo wa vyama vingi na kukifanya chama cha Tanu kushika hatamu za uongozi.
Mbali na kufutwa kwa mfumo huo, pia uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa asasi za kiraia ulidhoofishwa huku jumuiya mbalimbali za kiraia zikichukuliwa na kuwa jumuiya za Tanu.
Hata hivyo, hatua hiyo haikuwafurahisha baadhi ya watu akiwemo James Mapalala ambaye kwa wakati huo alikuwa ni mwalimu.
Mapambano yalipoanza
Akizungumza maisha yake hivi karibuni, Mapalala anasema aliamua kupambana na mfumo huo kutokana na ukandamizwaji wa haki za binadamu uliokuwa ukifanywa na Serikali tangu ngazi za juu hadi chini.
“Nilianza mapambano yangu rasmi mwaka 1968 wakati huo nikiandika makala katika Gazeti la Kiongozi wakati huo nikiwa naishi Tabora. Nilieleza kutoridhishwa na mateso wanayopata wananchi wakati huo ingawa kwa kweli Mwalimu Nyerere alikuwa na nia njema tu,” anasema Mapalala na kuongeza:
“Viongozi wa vijiji wakati ule walikuwa wakitesa wananchi na mimi niliandika kila kilichotokea.”
Kutokana na hali hiyo Mapalala alijikuta matatizoni na kufungwa jela katika gereza la Uyui na huo ulikuwa ni mkasa wa kwanza.
“Mkuu wa mkoa wakati huo akiitwa Makinda ambaye ni baba wa spika wa sasa, Anna Makinda, aliniweka jela.
Nilikaa kwa muda fulani hadi maaskofu na mashehe wa mkoa huo waliponihurumia na kumwandikia barua Mwalimu Nyerere kumwomba nitolewe,” anasema.
Anasema ombi hilo lilikubaliwa na Mwalimu Nyerere na hivyo kutolewa.
Hapo alifungua ukurasa mwingine ambapo kutokana na taaluma yake ya ualimu, aliomba na kupata kazi katika Shirika na la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) mwaka 1971.
“Nilitakiwa kwenda kufundisha Nigeria, hivyo nikaenda kuripoti kisha nikarudi ili niichukue familia yangu. Niliporudi, Jumapili moja nikiwa kanisani pale St. Peter, Oysterbay nikakutana na Nyerere… akaniita na kuniuliza, ‘nasikia unataka kuondoka?’ nikamjibu ni kweli. Akaniambia nisiondoke kuna kazi atanipa, hivyo niripoti ofisi za Tanu pale Lumumba siku iliyofuata,” anasema.
Anasema siku hiyo alipofika ofisini hapo, aliwakuta maofisa wa chama ambao walimpangia kazi ya kununua na kuuza ng’ombe kutoka mikoani.
“Niliifanya kazi ile kwa shingo upande kwa miaka miwili kisha nikaiacha. Hapo tena ile kazi yangu ya Unesco ikaota mbawa,” anasema.
Anasema tangu wakati huo alianza kufanya kazi zake binafsi ikiwa ni pamoja na kuwa mkandarasi wa majengo ambapo anasema aliwahi kupata zabuni ya kujenga maghorofa ya bandari.
Hata hivyo anasema ilipofika mwaka 1983, mapambano yake yakaanza tena ambapo wakati huo kulikuwa na mkutano wa wanasheria jijini Dar es Salaam ambao pia walimkaribisha.
“Wakati huo kulikuwa na wanasheria kutoka katika Chama cha Tanganyika Law Society walinialika kwenye mkutano uliokuwa ukizungumzia matatizo ya demokrasia nchini. Walizungumzia matatizo ya mfumo wa chama kimoja, lakini hawakutoa suluhisho. Mimi nilipendekeza uanzishwe mfumo wa vyama vingi nchini,” anasema Mapalala.
Hata hivyo, pendekezo hilo halikutiliwa maanani hadi mwaka 1984 wakati Chama Cha Mapinduzi kikiwa na mkutano mkuu ambapo Mapalala alifanya tena ‘uchokozi’ wake.
“Mwaka 1984 nilimwandikia barua Mwalimu Nyerere wakati wa mkutano mkuu wa CCM nikimtaka kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi. Hapo ndipo matatizo yakaanza kwani niliwekwa kizuizini. Nilikuwa nikihamishwa kutoka kituo kimoja cha polisi hadi kingine kwa karibu mwaka mmoja. Lakini zikufunguliwa kesi yoyote,” anasema.
Anaongeza kuwa mwaka 1986, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Muhidin Kimario alimkamata na kumfunga minyororo na kumpeleka kizuizini mkoani Lindi ambako alikaa hadi mwaka 1990 na wakati huo nilikuwa nikihamishiwa kisiwani Mafia.
Licha ya matatizo yote hayo Mapalala anasema hakukata tamaa na mawazo yake ya kuanzisha mfumo wa vyama vingi.
“Baada ya kutoka kizuizini, nilirudi tena na mawazo ya kuanzisha chama cha siasa. Nilikuwa na wenzangu ambapo tulianzisha chama wakati hakukuwa na sheria ya vyama vingi,” anasema na kuongeza:
“Hatukuogopa, tulikwenda kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, wakati huo Augustine Mrema na kumweleza haja yetu hiyo. Mrema alikuwa mkali sana akatufokea na kutufukuza.”
Baada ya kuona hivyo anasema waliamua kuandamana wakidai haki ya kuanzisha chama cha siasa,
“Tulikuwa watu 35 hivi, wakati maandamano yetu yanaanza. Tulipokuwa tukikaribia Kariakoo, watu waliongezeka na kufika hadi 1,000. Polisi wakaingilia kati na kuwakamata watu 25, mimi nikakimbilia Ubalozi wa Sweden kujificha.”
Anaendelea kusema kuwa, wale wanachama waliokamatwa na kupelekwa mahabusu waligoma kula kwa siku kadhaa na kuanza kuitisha Serikali.
“Ilibidi Serikali ije kuniomba niwasihi wale chakula. Ikabidi kitolewe chakula kizuri tena kutoka Kilimanjaro Hotel na kupelekwa gerezani na kuwabembeleza kula,” anasema.
Wakati mivutano hiyo ikiendelea, tayari kulishaanza kujitokeza mabadiliko ya kisasa na kiuchumi ulimwenguni ambapo mfumo wa ukomunisti ulianza kuanguka.
Kuanzisha, kufukuzwa CUF
Baada ya misukosuko ndipo walianzisha chama chao rasmi kikitwa Chama cha Wananchi (CUF) mwaka 1991.
Baada ya Serikali kupitisha sheria ya vyama vingi mwaka 1992, Mapalala anasema wanaharakati wengine wa mageuzi walikutana ukumbi wa Diamond Jubilee mwaka huo na kuanzisha chama cha NCCR-Mageuzi.
Hata hivyo, anasema mwaka huo kulikuwa na chama kingine huko Zanzibar cha ZUF (Zanzibar United Front) ambacho kilitaka kuunganisha nguvu na chama cha bara ili kiwe cha kitaifa.
“Walipokuja bara kuangalia chama chenye nguvu, wakaridhika na chama chetu na kuomba tuungane. Halmashauri kuu za vyama vyetu zikakaa kujadili suala hilo na hatimaye kukubaliana. Mwaka 1993 niliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CUF iliyoungana,” anasema.
Baada ya hapo anasema alifanya ziara katika mikoa karibu yote ya bara na Zanzibar kwa ajili ya kukitangaza chama hicho.
Hata hivyo, bahati haikuwa yake, anasema ilipofika mwaka 1994 mambo yakabadilika kwani wenzake hasa viongozi wa Zanzibar wakamgeuka na kuanza kumtuhumu kuwa anakisaliti chama.
Lakini mwenyewe anasema ilikuwa ni sababu za kidini pamoja na mkono wa Serikali uliokuwa ukiendelea kumwandama.
“Nilifukuzwa CUF kwa sababu za kidini tu. Ilikuwa mwaka 1994 baada ya kukijenga chama hicho nikashangaa mambo yamebadilika na viongozi wenzangu wamenigeuka. Wakawa wananishutumu kuwa natumiwa na CCM, mara nimechana bendera za chama, na tuhuma nyingi tu. Lakini nilipata hadi nyaraka zilizothibitisha sababu za udini,” anasema na kuongeza:
“Wakati huo CUF ilikuwa ikifadhiliwa na nchi za kiarabu, kwa hiyo wakasema ‘mtatakaje msaada wakati chama kinaongozwa na kafiri?’ Ndipo vituko vikaanza. Lakini hata Serikali pia ilichangia, nakumbuka siku ya mkutano wa kunifukuza kule Tanga, Msajili wa vyama vya siasa wakati huo, George Liundi alikuwepo hadi saa tisa za usiku akishadadia kufukuzwa kwangu.”
Baada ya kufukuzwa Mapalala akaanza upya tena mikakati ya kuanzisha chama kingine. Hata hivyo ilimchukua muda mrefu hadi mwaka 2003 ambapo alianzisha Chama cha Haki na Ustawi alichonacho hadi sasa.
Tangu alipokianzisha alifanikiwa kupata diwani mmoja tu mkoani Mara mwaka 2005 ambaye hata hivyo hakuendelea baada ya kumaliza miaka yake mitano.
Mapalala anazungumzia pia tukio la kunyang’anywa nyumba aliyokuwa akiishi maeneo ya Morocco jijini Dar es Salaam kwa amri ya mahakama mwaka 2010, na kulihusisha na misukosuko aliyoipata katika harakati za kuleta mageuzi nchini.
“Hapa unapoona ninaishi kwenye mabanda ya ng’ombe, baada ya nyumba yangu kubomolewa kwa amri ya mahakama, yaani ni misukosuko tu. Chama changu kinanitegemea kifedha lakini kwa hali hii inaniwia vigumu kukisaidia,” anasema.
Anazungumziaje upinzani wa sasa?
Akizungumzia vyama vya upinzani vya sasa, Mapalala anasema kuwa vimejikita zaidi kwenye kutafuta madaraka badala ya kueleza sera zao kwa wananchi.“Tofauti kati ya upinzani tuliokuwa tukiupigania miaka ile na wa sasa, ni watu kuwa na mawazo ya kwenda Ikulu tu bila kusema watawafanyia nini wananchi baada ya kufika huko. Hata kwenye chama tawala, CCM, hali ni hiyo hiyo, watu wanalilia tu Ikulu. Sisi tunasisitiza sera tu… sera nzuri ndiyo zitakazouza chama, chema chajiuza kibaya chajitembeza,” anasema.

Mwananchi

Serikali yatangaza nafasi za kazi 1,100

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imetangaza nafasi za kazi 1,134 katika sekta mbalimbali za ofisi za umma.
Kwa mujibu wa Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Xavier Daudi nafasi hizo za kazi ambazo zinapatikana katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira ya www.ajira.go.tz ni kwa ajili ya waajiri mbalimbali wa ofisi za umma.
Katibu alifafanua kuwa nafasi 949 ni kwa ajili ya waajiri walioainishwa katika ofisi za wizara, halmashauri na nyingine 185 ni za taasisi na wakala mbalimbali za Serikali.
Aidha, amewataka waombaji wote wa fursa za ajira kufungua matangazo yote mawili ya kazi na kuzingatia masharti ya Matangazo yote kama yalivyo katika lugha ya Kiingereza na Kiswahili kabla ya kutuma maombi yao Aprili 9, 2013.
Daudi alifafanua kuwa waajiri ambao watatoa ajira hizo ni makatibu wakuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha, Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi na Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Maendeleo Jinsia na Watoto, Wizara ya Kazi na Ajira na Ofisa Mtendaji Mkuu Wakala wa Vipimo.
Wengine ni Makatibu wakuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Ardhi Nyumba na Makazi, Wizara ya Maji na Katibu Ofisi ya Rais Maadili.
Wengine ni Makatibu Tawala wa Mikoa ya Kagera, Iringa, Ruvuma, Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Manyara, Dar es Salaam, Morogoro, Geita, Pwani, Mara, Kilimanjaro, Lindi, Singida, Tabora, Tanga, Katavi na Arusha; pamoja na wakurugenzi wa halmashauri za majiji na manispaa Mwanza, Iringa, Songea, Shinyanga, Morogoro, Singida, Kigoma/ Ujiji na Temeke.
Nafasi nyingine ni kwa ajili ya wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya Mufindi, Kyela, Rungwe, Mbeya, Chunya, Biharamulo, Bukoba, Muleba, Namtumbo, Songea, Morogoro, Makete, Mkuranga, Mbinga, Tunduru, Ukerewe, Sengerema, Ilemela, Busega, Maswa na Meatu.
Nyingine ni Wilaya za Shinyanga, Kishapu, Kilosa, Msalala, Rufiji, Rorya, Ruangwa, Lushoto, Mkinga, Mpanda, Monduli, Ngorongoro, Kigoma, Nachingwea, Rombo, Same, Singida, Urambo, Tabora, Babati, Mbulu, Simanjiro na Kiteto.
Pia zimo Wilaya za Handeni, Pangani, Kibondo, Chamwino Mtwara, Nanyumbu, Mpwapwa, Kongwa na Tandahimba pamoja na halmashauri za miji ya Njombe na Kibaha. Nafasi nyingine ni za Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita) na Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa).
Nafasi hizo zilizotangazwa zimegawanyika katika kada zifuatazo; Mchambuzi Mifumo ya Kompyuta daraja la II – (nafasi 10), Ofisa Vipimo II – nafasi 6, Mpima Ardhi, daraja la II (nafasi 26), Mhandisi daraja la II – Ufundi Umeme – Nafasi 9, Ofisa Mipango Miji daraja la II– nafasi 13 na Mhandisi daraja la II - Ujenzi (Nafasi 16).
Pia wanahitajika wahandisi daraja la II - Maji (Nafasi 13), Ofisa Misitu daraja la II (nafasi 7), Ofisa wa Sheria daraja la II – nafasi 3, Mtakwimu daraja la II – nafasi 8 na nyingine mbalimbali.

Tiketi zinatia najisi soka la Tanzania

MWAKA mpya 2014 ulianza kwa matumaini makubwa miongoni mwa wadau wa soka kwamba maendeleo yamefikiwa, ambapo ilitarajiwa Tanzania ianze kutumia tiketi za elektroniki.
Tiketi hizo zilianza kutumika lakini yalikuwa majanga, teknolojia ikakataa au wadau wakashindwa kuiweka inavyotakiwa.
Sintofahamu hiyo imeturudisha kule kule kwenye tiketi za vishina, ambapo kuna wanaofaidi kwa kukaa milangoni.
Nimeambiwa kuna jamaa wana vishina vya mechi zilizopita baina ya Yanga na Al Ahly na kwamba si ajabu hata mechi ijayo watavitumia au kurekebisha kidogo tu.
Soka imekuwa sehemu ya kwenda kula na si sehemu ya kwenda kutumia uzalendo, elimu, ujuzi na maarifa kuhakikisha sekta hii nayo inakua kiteknolojia na kulifaidisha taifa kiuchumi.
Tiketi za elektroniki ni hatua moja ndogo tu ya kuendea usasa zaidi, kwa sababu wenzetu huku wanabofya kwenye mtandao wa kompyuta, kulipia na kupata tiketi. Tutaona baadaye mifumo yao, manufaa na mapungufu kama yapo.
Kwetu Tanga yalikuwa maafa zaidi maana milango ya elektroniki haikuwafungulia washabiki waliofika Mkwakwani na inaelezwa zaidi ya nusu ya washabiki waliingia bure.
Wapo watu hata ndani ya mfumo wa uongozi wa soka katika klabu, mikoa na ngazi ya taifa wanapendelea mfumo wa kuchana tiketi pale mlangoni.
Ndiyo maana nachelea kusema kwamba mfuko wa elektroniki umekwama bali labda itakuwa sahihi zaidi kusema umekwamishwa.
Zipo tetesi pia kwamba Wachina walipokuwa wakijenga Uwanja wa Taifa ambao ni wa kisasa zaidi Afrika Mashariki walitoa wazo la kuweka mfumo huo moja kwa moja lakini ‘wadau wa maendeleo’ wakakataa. Kisa? Wanajua wao.
Kwa hali ilivyokuwa mbaya, wakati Ligi Kuu Tanzania inaanza kuhusiana na suala la tiketi, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) halikuwa na la kufanya zaidi ya kuzuia matumizi ya tiketi hizo. Niseme tu kwamba kuna watu waliopinga tangu awali tiketi hizo na wataendelea kupinga nyingine zozote zenye mfumo wa kuziba mianya ya wizi.
Wenzetu hapa Uingereza na mataifa mengine yaliyoendelea kisoka, ambayo hatuna budi kuyaiga katika mazuri yao, wanaoruhusiwa kuuza tiketi za mechi hapa ni klabu husika tu au mawakala wao waliopo kisheria na si kuchagua sijui vibanda vya soda au mikate Mwenge, Tandika au Ilala Bungoni.
Ni kosa kubwa kujihusisha na uuzaji wa tiketi ovyo, lakini kama ambavyo kuna wachumia tumbo hapo nyumbani, wapo hapa wanaojaribu kuzi upload tiketi kwenye tovuti mbalimbali na baadhi hudiriki kwenda karibu na viwanja na kuziuza kwa bei ya juu.
Bodi ya Ligi Kuu (Premier League) hapa England wamekuwa wakali sana wakishirikiana na mamlaka za dola kupambana kwa mafanikio makubwa na wauzaji feki wanaotundika tiketi kwenye tovuti na kuziuza na pia watu kadhaa wamedakwa na kushitakiwa kwa kuzilangua viwanjani.
Hili, pengine sawa na linaloweza kuwa limetokea au litatokea nyumbani, linakwenda sambamba na uuzaji wa tiketi za kughushi, ndiyo maana kama kuna kitu kinasisitizwa sana kwenye nchi hizi ni kununua tiketi (na bidhaa nyingine zozote) kwa mhusika halali na kupata stakabadhi.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inaposisitiza ukinunua dai stakabadhi na ukiuza toa stakabadhi, ni jambo ambalo huku ni la lazima, hata kama hutaki utajikuta umechanganyiwa stakabadhi ama na bidhaa zako au na chenji.
Klabu mwenyeji huuza tiketi zake lakini huwawekea wageni idadi wanayokubaliana na hutolewa mapema, iwe ni mechi ya Ligi Kuu au ya kimataifa na wala hutaona mkanganyiko.
Tiketi zikisemwa zimeisha basi shabiki ambaye angetaka kwenda uwanjani anashauriwa abaki nyumbani, atazame kwenye televisheni na kuwahi kutazama mtandaoni ratiba ya mechi inayofuata anunue mapema tiketi yake awe nayo kibindoni.
Malalamiko ambayo yamepata kuwapo ni tiketi za baadhi ya mechi kuwa ghali sana, mojawapo ya klabu zenye aina hiyo ni Arsenal lakini watu wanaoingia Emirates ni karibu 60,000.
Bodi ya EPL kwa mfano, imekuwa ikisambaza matangazo kwa njia mbalimbali kuwaasa washabiki walio ng’ambo ambao wangependa kuingia England kutazama mechi za EPL kuwasiliana kwanza na klabu husika kwenye tovuti zao.
Ni tofauti kabisa na jamaa wa Mbeya City wanaopanda Coaster zao na kutinga Dar kwa ajili ya mechi dhidi ya Simba siku hiyo hiyo ya mechi pasipo kuwa na tiketi mkononi, maana watazipata tu uwanjani na wanasema uwanja haujai, kwani eti si sawa na ndoo ya maji.
Premier League pia inatoa angalizo kwa washabiki hao, hasa wa ng’ambo kupendelea zaidi kununua tiketi kutoka kwa klabu husika ili kujiridhisha kwamba ni halali.
Ununuzi wote huo ni kwa mtandao, ambao rafiki zangu wa Tanzania watakuwa hawaupendi.
Tiketi za mechi za EPL zina soko sana kutokana na washabiki wengi kupenda kwenda wenyewe uwanjani kujionea mechi na wachezaji wawapendao, hata kwa kusafiri umbali mrefu.


I.G.Saria,
M: +44 (0) 7791284317
E: saria@tanzaniasports.com

Tunachojidanganya kuhusu Kaseja na Dida

SAYANSI ya soka la Tanzania ni tofauti na sayansi ya soka lolote ulilowahi kusikia duniani. Kuna wakati unajaribu kujiuliza tunatumia sayansi gani katika soka la kisasa lakini unaishia kukosa jibu.
Kwa mara ya kwanza nimesikia kuwa Tanzania kuna kipa wa mechi za ndani za ligi, na kuna kipa wa mechi za kimataifa. Hauwezi kuipata hii kokote duniani. Zamani na hata sasa tulizoea kusikia kipa wa dakika 90 na kipa wa kuja kucheza penalti baada ya dakika 120.
Lakini kuna sayansi mpya ya kipa wa mechi za kimataifa na kipa wa mechi za ndani. Ndivyo wanavyojidanganya watu wa benchi la ufundi au viongozi wa Yanga. Kwamba Juma Kaseja ni kipa waliyemsajili kwa ajili ya mechi za kimataifa wakati Deogratius Munishi ‘Dida’ ni kipa waliyemsajili kwa ajili ya mechi za ndani.
Katika soka halisi hakuna kitu kama hiki. Kipa wa mechi za ndani anapaswa kucheza mechi za kimataifa kwa sababu anacheza mechi nyingi kila mwisho wa wiki na ni rahisi kuwa fiti kuliko kipa wa mechi za kimataifa.
Kipa wa mechi za kimataifa anacheza mechi nne au sita tu kwa mwaka. Tangu lini kipa akacheza mechi chache kama hizi na akawa fiti kama si kumtafutia lawama?
Na hii si kwa kipa tu, bali kwa mchezaji yoyote uwanjani.
Kama Yanga wanataka kufanya vizuri katika mechi zao za kimataifa ni bora waendelee kumtumia Dida kwa sababu wakimtumia Kaseja watajikuta wanamlaumu bila ya sababu za msingi kwani naye anahitaji mazoezi yenye ushindani ili kulinda kipaji chake jambo ambalo kwa sasa analikosa .
Na kama wanataka Kaseja awe kipa wa mechi za kimataifa, basi huu ni wakati wa kuanza kumpanga mechi za ndani ili aendelee kuchangamka langoni.
Barani Ulaya, kipa wa kwanza anabakia kuwa kipa wa kwanza tu kwa sababu kadri anavyokumbana na mikikimikiki langoni ndivyo anavyoendelea kuimarika.
Kadri kipa yeyote anavyokaa nje ndivyo anavyoendelea kuporomoka kiwango chake taratibu bila ya kujifahamu.
Katika pambano la Jumamosi dhidi ya Al Ahly natazamia Kaseja kutocheza vema kama akipangwa kwa sababu uzoefu pekee hausaidii kiwango kizuri cha mchezaji.
 Mikikimikiki ya kila wiki inasaidia zaidi wachezaji hasa wa nafasi ya kipa. Kwa mshambuliaji haliwi tatizo kubwa sana.
Sir Alex Ferguson aliwahi kutaka kuwabadili makipa wake, David de Gea na Anders Lindergaard kadri awezavyo lakini mwisho wa siku alilazimika kukubali ukweli kwamba De Gea angecheza mechi karibu zote za Manchester United akiwa chaguo namba moja katika kikosi cha kwanza.
Na labda kwa ushauri mwingine kwa watu wa Yanga ni kwamba hawana sababu yoyote ya kumuharibia maisha kipa wao wa tatu, Ally Mustapha ‘Barthez’.
Huu ni wakati mwafaka wa kumruhusu kipa huyo aondoke klabuni kwao hata kama ana mkataba nao. kwani hawamtumii na hivyo anahitaji changamoto kupitia klabu nyingine ambazo zinahitaji huduma yake.
Kwa eneo la golikipa, daima unapaswa kuwa na makipa wawili wakubwa kama Dida na Kaseja. Kipa wa tatu anapaswa kuwa kipa kijana ambaye atakuwa ana maisha marefu klabuni huku akijifunza kutoka kwa wawili waliopo.
Kwa ilivyo sasa, Barthez hana cha kujifunza kutoka kwa Kaseja wala Dida. Hapo hapo unajaribu kuwaza kuwa kama Kaseja anasugua benchi vipi kwake yeye?  Uungwana mzuri sana ni kumruhusu aondoke kwenda kucheza katika timu ambayo atapangwa mara kwa mara.

Mwanaspoti

Al Ahly yakodi mpishi Mjerumani

KIKOSI cha timu ya soka ya Al Ahly ya Misri, kitafikia kwenye hoteli ya kifahari ya Kempinski jijini Dar es Salaam, lakini kwenye msafara wao watakuja na mpishi wao maalumu.
Timu hiyo ya Misri imepanga kutua Dar es Salaam leo Jumanne ingawa haijawapa taarifa Yanga na tayari maofisa wao wapo jijini wakiandaa mazingira.
Hata hivyo timu hiyo imezuga kwenye mitandao yao kwamba hawako vizuri kiuchumi kwa sasa na kwamba hata Sh112 milioni walizotumia kwa safari ya kuja nchini wamezipata kwa kuungaunga.
Al Ahly inayowasili na msafara wa watu 32 miongoni mwao wachezaji wakiwa 22 na viongozi 10, mpishi wao ni raia wa Ujerumani ambaye atashirikiana na wataalamu wa hoteli hiyo.
Timu hiyo ilizikataa hoteli tano za awali ilizotafutiwa na Yanga kwa madai kwamba zina vyumba vidogo. Ikiwatumia maofisa kadhaa wa ubalozi wa Misri nchini, Al Ahly iliamua kuchagua hoteli hiyo huku ikipata uwanja wa mazoezi katika Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST), Masaki sehemu ambayo ina ulinzi mkali na mashabiki hawaingii kirahisi.
Mkurugenzi wa Michezo wa Al Ahly, Sayyid Abdul Hafiyz,   alitarajiwa kuwasili jana Jumatatu kuungana na maofisa wengine waliotangulia.

Viongozi wa Simba wamepata msiba wa mjomba yupi?

UMEWAHI kuona rubani anaiteka ndege yake? Bila shaka unakumbuka kisa cha rubani msaidizi, Hailemedhin Abera (31) aliyeiteka ndege ya Ethiopian Airlines Jumatatu ya wiki iliyopita kwa madai ya kuwa na msongo wa mawazo kwa kufiwa na mjomba wake.
Abera, ambaye amefanya kazi kwenye shirika hilo maarufu la ndege kwa miaka mitano alijifungia kwenye chumba cha marubani baada ya rubani mkuu kwenda msalani.
Rubani huyo msaidizi ‘aliendesha’ ndege hiyo kwa saa sita na badala ya kuipeleka Roma, Italia aliipeleka Geneva, Uswisi ambako alitua baada ya kuomba kupewa hifadhi nchini humo.
Rubani huyo alifanya kituko kwa kuwatisha abiria kwa kuchomoa vikasha vya hewa ya oksijeni kwenye ndege hiyo na kutishia kuzima mfumo wa hewa iwapo abiria hao wasingekubali kufuata maelekezo yake.
Rubani huyo akawaambia abiria kwa ukali: “Kaeni chini, vaeni vikasha vya oksijeni kwenye viti vyenu, nitakwenda kukata mfumo wa hewa ya Oksijeni.”
Baada ya rubani huyo kuwazungusha abiria kwa saa sita angani wakiwa hawajui hatima yao, alitua Geneva na kushuka kupitia dirishani kwa msaada wa kamba huku akiomba hifadhi kabla ya kujisalimisha kwa polisi.
Ndege hiyo aina ya Boeing 767-300 iliyokuwa na abiria 201 na wahudumu iliondoka mjini Addis Ababa na kutua mjini Geneva, ikiwa imebakiza mafuta yanayayoiwezesha kuendelea kuwepo hewani kwa dakika 20 tu.
Si ndege tu ambayo inaweza kutekwa, hata viongozi wa Simba wamewateka nyara wanachama wao kwa kuitisha mkutano mkuu Machi 16 ambao utajadili ajenda moja tu ya mabadiliko ya katiba.
Itakuwaje Simba yenye migogoro mingi iwe na ajenda moja tu ya kujadili mabadiliko ya katiba wakati wanachama wanataka kujua suala la uwanja wao wa Bunju B.
Itakuwaje ijadiliwe ajenda moja tu katika mkutano huo wakati wapo baadhi ya wanachama katika Simba ambao wanataka kujua Emmanuel Okwi aliuzwa vipi kwenda Etoile du Sahel ya Tunisia  bila malipo yoyote.
Wanachama wanataka kupata majibu inakuwaje Okwi licha ya ubora wake auzwe kwa mkopo na fedha haijalipwa mpaka sasa?
Wanachama wanataka kujua inakuwaje mchezaji wao kiraka Shomari Kapombe apelekwe AS Cannes ya Ufaransa kwa mkataba ambao hauna maelezo ya kujitosheleza.
 Kapombe, miongoni mwa wachezaji bora Afrika Mashariki na Kati sasa yupo nchini akiwa hajui hatima yake, lakini Simba wapo kama vile hawana shida naye.
Simba imecheza mechi nne na kupata pointi mbili tu, kuna tatizo gani hapo. Wanachama wanataka kupata majibu sahihi kuna tatizo gani katika timu hiyo?
Matatizo yote hayo yanapaswa kujadiliwa katika mkutano mkuu wa wanachama wa Simba na hasa ikizingatiwa kuwa kuna mgawanyiko mkubwa ndani ya uongozi na Kamati ya Utendaji.
Kwa misimu miwili mfululizo, Simba inashindwa kushiriki mashindano ya Shiriisho la Soka Afrika (CAF) iwe Ligi ya Mabingwa au Kombe la Shirikisho. Wanachama wanataka kujadili hayo.
Inawezekana Simba inataka kufika mahali fulani kuzuri, lakini viongozi wake wamewateka wanachama na wanawapeleka sehemu nyingine huku wakiomba hifadhi maalumu.
Yule rubani wa Ethiopia aliiteka ndege kwa madai alikuwa na msongo wa mawazo baada ya kufiwa na mjomba wake, sielewi viongozi wa Simba wamepata msongo wa mawazo baada ya kufiwa na mjomba yupi?

Mwanaspoti

Yanga, Simba milioni 100

MECHI za Ligi Kuu Bara zilizohusisha Yanga na Simba na kuchezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wikiendi iliyopita zimeingiza Sh101 milioni.
Yanga ambayo Jumamosi iliyopita iliichapa Ruvu Shooting mabao 7-0 mechi yake iliingiza Sh68.4 milioni kutokana na mashabiki 11,972 kuingia uwanjani.
Katika mechi hiyo kila klabu ilipata mgawo wa Sh15,687,488 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa kutokana na mapato hayo ni Sh 10.4 milioni. Gharama za tiketi ni Sh3.8 milioni na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) ilipata Sh 4.8 milioni wakati uwanja ulipata Sh8.1 milioni.
Gharama za mchezo zilikuwa Sh4.8 milioni wakati Mfuko wa Maendeleo ya soka (FDF) Sh2.4 milioni. Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA) na Chama cha Soka Pwani (COREFA) kila kimoja kilipata Sh945,110.
Simba na JKT Ruvu iliyochezwa juzi Jumapili na kushuhudiWa na watazamaji 5,850 iliingiza Sh32.7 milioni kwa viingilio vya Sh5,000, Sh 15,000 na Sh20,000. VAT iliyolipwa ni Sh4.9 milioni.
Kila klabu ilipata mgawo wa Sh7.4 milioni, tiketi ni Sh2.5 milioni huku gharama za mechi zikiwa Sh 2.2 milioni. Uwanja ulipata Sh3.7 milioni wakati TPLB walipata Sh2.2 milioni. Mgawo mwingine ni FDF Sh1.1 milioni na DRFA Sh881,376.

Monday 24 February 2014

VYUO VIKUU 100 BORA AFRICA

VYUO VIKUU 100 BORA AFRICA
1 Cairo University
Egypt
2 University of Cape Town
South Africa
3 University of Pretoria
South Africa
4 Universiteit Stellenbosch
South Africa
5 University of South Africa
South Africa
6 University of the Witwatersrand
South Africa
7 University of the Western Cape
South Africa
8 Ain Shams University
Egypt
9 Alexandria University
Egypt
10 Mansoura University
Egypt
11 University of KwaZulu-Natal
South Africa
12 University of Dar es Salaam
Tanzania
13 The American University in Cairo
Egypt
14 Rhodes University
South Africa
15 Assiut University
Egypt
16 Université Mohammed V – Agdal
Morocco
17 University of Nairobi
Kenya
18 Université de Ouagadougou
Burkina Faso
19 University of Johannesburg
South Africa
20 Makerere University
Uganda
21 University of Botswana
Botswana
22 Zagazig University
Egypt
23 University of Ghana
Ghana
24 Universidade Eduardo Mondlane
Mozambique
25 Obafemi Awolowo University
Nigeria
26 University of Khartoum
Sudan
27 Université Mentouri de Constantine
Algeria
28 Université de la Reunion
Reunion
29 Benha University
Egypt
30 The German University in Cairo
Egypt
31 Université Cheikh Anta Diop
Senegal
32 Addis Ababa University
Ethiopia
33 North-West University
South Africa
34 Sudan University of Science and Technology
Sudan
35 Université Abou Bekr Belkaid Tlemcen
Algeria
36 University of Namibia
Namibia
37 Al Akhawayn University
Morocco
38 College of Arts and Social Sciences, University of Rwanda
Rwanda
39 University of Lagos
Nigeria
40 Helwan University
Egypt
41 Université Mouloud Maameri de Tizi Ouzou
Algeria
42 Université de Batna
Algeria
43 Nelson Mandela Metropolitan University
South Africa
44 University of Zimbabwe
Zimbabwe
45 University of Zambia
Zambia
46 Université Abdelhamid Ibn Badis Mostaganem
Algeria
47 Université Abdelmalek Essadi
Morocco
48 Université d’Alger
Algeria
49 Université d’Antananarivo
Madagascar
50 Moi University
Kenya
51 Université Mohammed V – Souissi
Morocco
52 South Valley University
Egypt
53 Minia University
Egypt
54 Tanta University
Egypt
55 Al-Azhar University
Egypt
56 Cape Peninsula University of Technology
South Africa
57 University of Ilorin
Nigeria
58 Minoufiya University
Egypt
59 Université M’hamed Bouguerra de Boumerdes
Algeria
60 Université d’Oran
Algeria
61 Suez Canal University
Egypt
62 Kwame Nkrumah University of Science and Technology
Ghana
63 Université Cadi Ayyad
Morocco
64 Federal University of Technology, Minna
Nigeria
65 University of Swaziland
Swaziland
66 Université Ibn Tofail
Morocco
67 Strathmore University
Kenya
68 Université Hassan II Mohammedia – Casablanca
Morocco
69 Kafr el-Sheikh University
Egypt
70 University of Ibadan
Nigeria
71 Université Hassan II – Casablanca
Morocco
72 University of Malawi
Malawi
73 Université des Sciences et de la Technologie Houari Boumediène
Algeria
74 Universiteit van die Vrystaat
South Africa
75 University of Nigeria
Nigeria
76 Universidade de Cabo Verde
Cape Verde
77 Polytechnic of Namibia
Namibia
78 Kenyatta University
Kenya
79 Libyan International Medical University
Libya
80 Ahmadu Bello University
Nigeria
81 University of Mauritius
Mauritius
82 Sirte University
Libya
83 Tshwane University of Technology
South Africa
84 University of Benin
Nigeria
85 University of Agriculture, Abeokuta
Nigeria
86 Durban University of Technology
South Africa
87 Université Kasdi Merbah de Ouargla
Algeria
88 Université de Sousse
Tunisia
89 Université de Tunis El Manar
Tunisia
90 University of Gezira
Sudan
91 University of Cape Coast
Ghana
92 Université de la Manouba
Tunisia
93 United States International University
Kenya
94 Covenant University
Nigeria
95 Central University of Technology
South Africa
96 Université Mohamed Khider de Biskra
Algeria
97 Madonna University
Nigeria
98 The British University in Egypt
Egypt
99 University of Fort Hare
South Africa
100 Sokoine University of Agriculture
Tanzania

Magazeti ya leo February 24 2014 Udaku, Michezo na Hardnews



.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.