Monday 3 February 2014

Moyes:Manchester United haina habati


Meneja wa Manchester United David Moyes anahisi kuwa klabu yake isingekosa bahati hivyo kiasi cha kupata kichapo cha mabao mawili kwa moja dhidi ya Stoke City.
Ni mechi yao ya nane kushindwa katika ligi kuu msimu huu.
Charlie Adam aliwawezesha wenyeji kupata ushindi kwa bao la kwanza na kisha kuingiza bao la pili baada ya Robin van Persie kupatia Man U bao la kufutia machozi.
"sijui tufanyeje tuweze kushinda,'' alisema Moyes baada ya mechi. Nadhani tu hatuna bahati hata kidogo.''

Tulicheza vyema, lakini kwa bao la kwanza la wenyeji lilitokana na Man U la pili pili lilikuwa la kubahatisha,'' aliongeza Moyes.
Mchezaji aliyesajiliwa hivi karibuni, Juan Mata, Van Persie na Rooney wote walicheza katika kikosi cha kwanza kilichoshambulia sana Stoke.
Van Persie alisaidia Man U kwa bao lake na kwa mchezo mzuri ingawa walishindwa tu kuingiza mabao.
Licha ya shinikizo kutoka kwa Man U, bahati haikuwa yao.
"tulikuwa na nafasi nzuri za kuingiza mabao lakini haikuwezekana,'' alisema Moyes
"ndio, Wayne alikaribia kuingiza bao , ingawa ilikuwa vigumu kwa mabao.Tungestahili kupata mabao kutokana na wachezaji walivyocheza, yaani tujilaumu sisi wenyewe tu,'' aliongeza Moyes.
United wangali katika nafasi ya saba kwenye jedwali la pointi, wakiwa nyuma kwa pointi kumi na tatu dhidi ya Man City wanaoongoza jedwali hilo ambao watacheza na Chelsea Jumatatu.
Pia wako nyuma ya Liverpool ambao ni wa nne kwa alama sita .

No comments:

Post a Comment