Monday 12 May 2014

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii


Dengue: Unayohitaji Kujua
Dengue ni ugonjwa unaoleta homa kwa muda wa siku 2 hadi 7 na huambatana na dalili zifuatazo:
- Kuumwa kwa macho.
- Kuumwa kwa kichwa.
- Maumivu ya misuli na viungo.
- Kutokwa na damu (katika fizi au pua).
- Kukwaruzika kwa urahisi.
Huduma ya nyumbani kwa homa ya Dengue ni:
- Pata vinywaji kwa wingi mfano maji, juisi au chai.
- Tumia dawa za maumivu kupunguza homa.
- Usitumie dawa ya "Aspirin" ama "Ibuprofen"
Nenda hospitali haraka unapoona moja ya dalili za tahadhari. Dalili za tahadhari za kuangalia baada ya homa kuondoka:
- Maumivu makali ya tumbo.
- Kutapika mfululizo.
- Kutokwa damu.
- Ngozi kupauka na kuwa baridi.
- Kudhoofika kwa mwili, usingizi mzito.
- Kizunguzungu, kuzimia.
- Kupumua kwa shida.

No comments:

Post a Comment