Sunday 29 September 2013

UISLAMU NI UGAIDI AU PROPAGANDA ZA WAHALIFU?


Wengine mnaweza msinielewe, na hamtanielewa kwa sababu tu ya kasumba na taarifa mlizolishwa na watu, na hasa watu wenye mamlaka kwenu, na sana sana hawa wanaweza kuwa viongozi wa dini mnaowaamini.

UGAIDI NA UISLAMU: Wapo watu wanaojaribu kutaka tuamini na kukubaliana nao kwamba eti uislamu ni ugaidi, au waislamu ni magaidi duniani.

MIMI: Naam bado sikubaliani na bado siamini kuwa eti Uislamu ni ugaidi, ninachojua ni kwamba hii ni mbinu chafu ya watu fulani, wenye maslahi fulani wanaotaka kutumia jina la Uislamu kutekeleza uhalifu kwa lengo la kufikia malengo yao.

Na njia pekee ya kufikia malengo yao ni kufanya vitendo vitakavyowajengea watu hofu katika jamii, na pili kuwagawa watu kwa misingi ya udini na siasa ili kutekeleza na kupata maslahi wanayoyataka.

No comments:

Post a Comment