Wednesday 29 January 2014

FURAHA YARUDI MAN UTD, MATA AFUNIKA


Juan Mata ametoa mchango mkubwa lakini cha kukumbukwa zaidi ni pasi yake ya bao la pili lililofungwa na Ashley Young mnamo dakika ya 53.

Kabla ya hapo, Robin van Persie aliyekuwa amerejea akitokea kuuguza majeraha, alifunga mapema bao la kwanza takribani dakika ya 6.

Baadaye van Persie alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Wayne Rooney ambaye pia alikuwa majeruhi!

No comments:

Post a Comment