Monday 20 January 2014

Ndoa ya Obama, Michelle shakani

Marekani. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa vyanzo vya ndani vya Ikulu ya Marekani, wenza hao wamekuwa katika migogoro na Obama alilazimika kusherehekea sherehe za mwaka mpya mjini Hawaii akiwa na binti zake wawili, Sasha na Malia bila kuwepo Michelle.
Jarida la National Enquirer lilieleza kwamba katika moja ya matukio, Obama aliwahi kukutwa akiwa na mwanamke mwingine katika ‘mazingira ya kutatanisha’ wakati mkewe akiwa safarini.
Kutokana na ripoti iliyotolewa na Bombshel , Michelle na Obama wamekuwa wakilala vyumba tofauti ndani ya Ikulu. Michelle pia anajiandaa kuhama katika jumba lao pale Chicago ambalo wameishi wakati wa uchumba wao miaka 21 iliyopita na kwa msisitizo watajadili juu ya talaka.
Taarifa ilidai tatizo limeanza miaka minane iliyopita pale Obama alipodhamiria kujijenga kisasa. Ni mtoto wao Sasha ambaye aliumwa ugonjwa unaosababishwa na woga wa maisha unaoitwa Spinal Meningitis ndiyo uliowafanya waendelee kuwa pamoja.
Kitabu cha Anderson kinaelezea tatizo lilivyoanza baada ya Barack Obama kuamua kuingia kwenye siasa, ambapo Michelle alisikika akimwambia mumewe; “Wewe unajifikiria mwenyewe tu.”
Naye Barack Obama amesikika akisema: “Sikuwahi kufikiri kamwe kwamba ningelea familia mwenyewe siku moja.” Anderson anadai kuwa Obama amechoshwa na malalamishi ya mkewe.
“Nampenda sana Michelle lakini ananiumiza na ubishi wake wa kila mara,” alisikika akisema Obama na kuongeza kuwa; “Anaonekana ni mwingi wa machungu na hasira siku zote.”
Akizungumza na televisheni ya CBS ya Marekani, Anderson alidai kuwa ilikuwa nusura Michelle atembee nje ya ndoa kwa sababu ya upweke.
Kwa miaka mitano wamekuwa na wasiwasi juu ya uwezo wao wa kupata watoto kabla Malia hajazaliwa. Walishajadili sana suala la kuasilia watoto (adoption) na marafiki zake wa karibu lakini kwa bahati nzuri Malia alizaliwa mwaka 1998 na kuondoa wazo hilo.
Jina kamili la Obama ni Barack “Barry” Hussein Obama, Jr, alizaliwa Agosti 4, 1961 Honolulu, Hawaii, alikulia huko huko Hawaii na Indonesia, baba yake mzazi ana asili ya Kenya. Jina kamili la mkewe ni Michelle LaVaughn Robinson, alizaliwa Januari 17, 1964 Chicago, Illinois.
Kukutana kwako
Barack na Michelle walikutana mwaka 1989 katika mazingira ya kikazi, walifunga ndoa Oktoba 18, 1992, katika Kanisa la Umoja wa Kristu la Trinity lililopo Chicago, Illinois.

No comments:

Post a Comment