Monday 2 December 2013

TAMKO LA MWENYEKITI WA CHADEMA MKOA WA LINDI NA KATIBU OFISI YA KATIBU MKUU- SEKRETARIET‏

Ally Omary Chitanda akitoa salaamu zake kwa wananchi katika mkutano.
ALLY OMARY CHITANDA
MWENYEKITI WA CHADEMA
MKOA WA LINDI
30/11/2013
KATIBU WA CHADEMA
MKOA WA LINDI
YAH; KUJIUZURU UENYEKITI WA MKOA
Somo la hapo juu lahusika.
Napenda kuchukua nafasi hii kukuarifu kuwa kwa hiari yangu bila ya kushawishiwa na mtu yeyote, nimeamua kujiuzuru nafasi ya Uenyekiti wa Mkoa tangu leo tarehe 30/11/2013.
Nashukuru sana kwa ushirikiano wako pamoja na Vionmgozi wote wa Baraza la Uongozi pamoja na Baraza la Mashauriano la Mkoa, lakini pia niwashukuru Viongozi wote wa Majimbo naWilaya hasa Nachingwea ambao kwa kiasi kikubwa, wameniwezesha kufika hapa hasa wakati mgumu wa Ujenzi wa Chama  na  kugombea Ubunge 2005 na 2010.Matarajio yangu ya kuweza kukomboa wanyonge kupitia CHADEMA kwa sasa  sioni kama yanaweza kufikika.
Nitabaki kuwa Mwanachama wa kawaida na ninaahidi kuwa Mwanachama  mwaminifu na pale  nitakapohitajika  nikotayari  kusaidiana na Viongozi  kujenga Chama.Nawataki kazi njema na Ujenzi wa Chama.

Ahsante kwa ushirikiano.
………………………………..
A.O. CHITAND

No comments:

Post a Comment