Tuesday 29 October 2013

Al Ahly kukutana na Orlando Pirates


Klabu ya soka ya Misri, Al-Ahly iko kifua mbele katika kutetea ubingwa wao wa ligi ya klabu bingwa Afrika baada ya kuicharaza klabu ya Cameroon ya Coton Sport katika penalty ili kuweza kufika fainali.
Klabu hiyo ya Cairo ilishinda kwa ujumla wa mabao sita saba kwenye mechi iliyochezwa katika eneo la El-Gouna baada ya mechi ukamilia kwa sare ya bao maoja kwa moja.

Matokeo sawa na hayo yalishuhudiwa kwenye mechi ya mkondo wa kwanza, iliyomalizika kwa mabao mawili kwa mawili.
Ahly itakutana na Orlando Pirates wa Afrika Kusini katika fainali itakayokuwa na mikondo miwili mwezi ujao.
Abdullah Al Saied aliingiza bao baada ya dakika tatu ya kuanza kwa mchezo na kuipa Misri mwanzo mzuri wa mechi , na kisha kuingiza bao lengine.
Ahly, ambayo haikushiriki mechi tatu za kimataifa, iliyohusisha mechi ya Misri ambayo ilishindwa vibaya sana na Ghana, ilipata nafasi nzuri za kuendeleza ushindi wao wakati wa kipindi cha kwanza cha mchuano.
Mchezaji Alexis Yougouda alifanikiwa kuingiza bao lake la saba
Wakati wa mchuano huo, Mohamed Aboutrika alikosa bao lake la kwanza lakini wachezaji wenzake walifanikiwa kuingiza mabao baadaye.
Mechi hiyo ilichezwa bila ya mashabiki baada ya kupigwa marufuku kushuhudia mechi za klabu yao, kutokana na ghasia za hivi karibuni.
Kocha wao Mohamed Youssef pia alilazimika kujionea mechi akiwa nje ya uwanja baada ya kuondolewa uwanjani wakati wa mkondo wa kwanza wa mecih hizo mjini Garoua wiki mbili zilizopita.
Ahly wameshinda ubingwa wa ligi hiyo mara saba awali, na kuifanya kuwa klabu yenye kufanikiwa zaidi barani Afrika.

No comments:

Post a Comment