Friday 25 October 2013

Alex Ferguson kumsaidia kocha David Moyes

Manchester, England. Kocha wa zamani wa Manchester United, Alex Ferguson amesema atampa ushirikiano wa kutosha kocha wa sasa wa Manchester United, David Moyes.
Ferguson alisema hayo wakati alipokuwa akizindua kitabu chake ambacho kimewakosoa nyota wengi aliokuwa nao Manchester United kama Roy Keane, David Beckham, Wayne Rooney, Carlos Tevez na Anderson.
“Mimi nilipojiunga Manchester United nilipewa ushirikiano wa kutosha na Matt Busby, alinisaidia sana, ninatarajia kumsaidia David Moyes kama mimi nilivyosaidiwa na Busby,” alisema Ferguson.
Kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu msimu huu kocha Moyes alisema ratiba siyo nzuri kwa upande wa Man U kwani katika mechi zake tano za mwanzo ilipangiwa kucheza na Chelsea, Liverpool na Manchester City. Akizungumzia hilo kocha Ferguson alisema,”hata mimi nilipoiona ratiba ya msimu huu niliona Manchester itakuwa na wakati mgumu mwanzoni mwa msimu.”
Alisema,”Hata hivyo watu wengi wanasahau Man U ni timu ambayo inaweza kutoka chini na kupanda mpaka juu na kutwaa ubingwa.”

No comments:

Post a Comment