Monday 28 October 2013

Viwanja vya mamilioni vyauzwa Mapinga

Viwanja hivyo vinauzwa kwa bei ya kuanzia Sh10 milioni na kuendelea .
Dar es Salaam. Taasisi ya Dhamana ya Uwekezaji Tanzania, (UTT) imeanza kuuza viwanja kwa wananchi  katika eneo la Mapinga wilayani Bagamoyo.
Lengo ni kurahisisha maendeleo kwa wananchi kwa kuwa na viwanja  bora vilivyounganishwa na miundombinu ya maji, umeme na barabara. Pia kuongeza thamani ya mji wa Bagamoyo unaotarajia kuwa na bandari Msanifu Mwandamizi wa mradi huo kutoka UTT, Godfrey Mwakabole ,alisema  katika mradi wa kwanza viwanja 246 ambavyo vimepimwa na kuwekewa huduma zote muhimu za barabara, maji na umeme vitauzwa kwa wananchi.
Mwakabole aliyasema hayo jana wakati wa  uzinduzi wa mpango wa uuzaji wa viwanja hivyo.
 “Eneo zima la mradi huu  wa Mapinga lina viwanja 1,000 na UTT  tayari tumesha anza kuuza viwanja 246 na  awamu ya pili ya mradi huu itakuwa ya  kujenga nyumba ambazo zitauza kwa bei nafuu,”alisema Makabole.
Alisema  kiwanja cha bei ya nchini kitakuwa Sh10 milion na kwamba  mradi wa kwanza utakamilika mwaka 2015.
Ofisa Mkuu wa Usimamizi wa mradi,  Shakiru Abdulkarimu  alisema UTT inashirikiana na manispaa katika upimaji wa viwanja katika maeneo mbalimbali.
Alisema tayari Manispaa ya Bukoba imeshapima viwanja 5000 na upimaji wa viwanja kama huo unaendelea Lindi na Mtwara.

No comments:

Post a Comment