Wednesday 21 August 2013

Wambura ajitoa uchaguzi TFF

Aliyewahi kuwa mgombea wa Uchaguzi Mkuu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) uliosimamishwa na Fifa, Michael Wambura, amesema hatashiriki tena kwenye uchaguzi ujao wa shirikisho hilo, Oktoba 27.
Awali Wambura, aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa FAT (sasa TFF), aliwania nafasi ya Makamu Rais katika uchaguzi uliosimamishwa na Shirikisho la Soka Ulimwenguni (Fifa), kutokana na kuwepo malalamiko kutoka kwa watu  walioenguliwa akiwamo yeye.
Jana TFF ilitangaza majina ya wagombea 58 wote ikiwa ndiyo siku ya mwisho  kurejesha fomu, lakini bila kuwepo kwa jina la Wambura ambaye  alipoulizwa na Mwananchi sababu ya kutogombea tena alisema: “Siwezi  kujisafisha na majitaka.”
“Nimeamua kupumzika, nilipigania haki imepatikana kwa kamati mbili kuundwa. Bila mimi kamati hizo zisingekuwapo, lakini jambo muhimu ni kwamba siwezi kujisafisha na majitaka,” alisema Wambura.
“Mfumo wa uongozi TFF ni mbovu, kumejaa siasa za majitaka, hizo kamati  zilizoundwa hazitafanya kazi kwa vile tu Wambura hayupo, ningekuwepo  zingepata kazi ya kufanya,” alitamba Wambura.
Wakati Wambura akiingia mitini, Jamal Malinzi amejitosa tena kuwania  nafasi ya Urais akichuana na Athuman Nyamlani, Omari Nkwarulo na  Richard Rukambura.
Nafasi ya Makamu wa Rais inawaniwa na Iman Madega, Ramadhan Nasib na  Walace Karia, huku wajumbe waliomba kuwakilisha kanda mbalimbali ni Abdallah Mussa, Kaliro Samson, Jumbe Magati, Mugisha Galibona, Vedastus  Lufano, Samwel Nyalla, Epaphra  Swai, Mbasha Matutu, Stanslaus Nyongo, Ally Mtumwa, Elley Mbise na Omari Walii. ni Ahmed Mgoyi, Yusuf Kitumbo, Ayoub Nyaulingo, Blassy Kiondo, Nazarius Kilungeja, Ayoub  Nyenzi, Cyprian Kuyava, David Lugenge, Elias Mwanjala, Eliud Mvela, John  Kiteve, James Mhagama, Kamwanga Tambwe na Stanley William Lugenge, Athuman Kambi, Francis Kumba, Zafarani Damoder.
Charles Komba, Hussein Mwamba, Stewart Masima, Farid Nahdi, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’, Riziki Majala, Twahil Twaha Njoki, Davis  Mosha na Khalid  Mohamed. Alex  Kamuzelya, Juma Pinto, Muhsin Balhabou, Omar Abdulkadir, Shaffih Dauda na Wilfred  Kidao. Kwa upande wa TPL Board waliojitokeza kuwania uongozi wa juu ni wawili Hamad Yahya (Mwenyekiti) na Said Muhamad Said (Makamu Mwenyekiti).Walioomba nafasi za ujumbe wa TPL Board ni Kazimoto Muzo, Michael  Kaijage, Omari Mwindadi, Salum Rupia na Silas Magunguma.

Chanzo Mwananchi

No comments:

Post a Comment